HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 23, 2018

Londoni Sekondari yashinda Mashindano ya Vilabu vya kodi shule za Sekondari Ruvuma

 Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018 linaloendelea Mkoani Ruvuma. Wengine kutoka kushoto ni Meneja wa TRA mkoa wa Ruvuma Rosalina Mwenda, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo na Meneja wa NMB Ruvuma Ritha Majahasi.
 Mwanafunzi kutoka shule ya Sekondari Londoni akipongezwa na Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro (wa pili kulia) baada ya shule yake kuibuka mshindi wa jumla wa mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018.
  Mwanaidi Hamisi mwanafunzi wa shule ya Sekondari Maposeni akipokea zawadi ya kibubu baada ya kuibuka mshindi wa pili katika shindano la uchoraji wa kibonzo kinachohusu masuala ya kodi.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo akimkabidhi kibubu ambacho ameweka fedha taslim shilingi 50,000 mmoja wa wanafunzi walioibuka washindi wa kuwasilisha vizuri mada kuhusu mashine za kodi za kielektroniki wakati wa mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari  katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018.
 Washindi wa jumla wa mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa Shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018 (waliosimama) wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo (wa pili kushoto), Meneja wa TRA Ruvuma Rosalina Mwenda (wa kwanza kushoto) na Meneja wa NBM Ruvuma Ritha Majahasi (wa kwanza kulia).

 Majaji (waliosimama) walioshiriki kuchagua shule bora na wanafunzi bora katika mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018 wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo (wa pili kushoto), Meneja wa TRA Ruvuma Rosalina Mwenda (wa kwanza kushoto) na Meneja wa NBM Ruvuma Ritha Majahasi (wa kwanza kulia).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad