Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akipewa tuzo ya Balozi wa amani na Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa wa Wabunge wapenda amani, Dkt. Thomas Walsh katika hafla ya kuzindua tawi la Wabunge wapenda amani iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (kushoto) akipewa tuzo ya Balozi wa amani na Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa wa Wabunge wapenda amani, Dkt. Thomas Walsh katika hafla ya kuzindua tawi la Wabunge wapenda amani iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
Spika
wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Waheshimiwa Wabunge (hawapo
kwenye picha) wakati wa hafla ya kuzindua tawi la Wabunge wapenda amani
iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri
Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (kushoto), Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa
wa Wabunge wapenda amani, Dkt. Thomas Walsh, Spika wa Bunge, Mhe. Job
Ndugai na Katibu Mkuu wa Chama cha Wapenda amani Duniani Afrika, Ndg.
Adama Doumbia wakifuatilia video inayoelezea mambo mbali mbali
yanayohusiana na amani katika tukio lililofanyika leo katika Ukumbi wa
Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
Wabunge
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wakiwa katika hafla ya kuzindua tawi la
Wabunge wapenda amani iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa
Bungeni Jijini Dodoma. Hafla hiyo Ilihudhuriwa na Mgeni rasmi Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (watatu kushoto), Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (watatu kulia), Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa wa Wabunge wapenda amani, Dkt. Thomas Walsh (wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya hafla ya kuzindua tawi la Wabunge wapenda amani iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (katikati) akisalimiana na Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa wa Wabunge wapenda amani, Dkt. Thomas Walsh (kushoto) baada ya hafla ya kuzindua tawi la Wabunge wapenda amani iliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Kulia ni Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai
(PICHA NA DEONISIUS SIMBA - OFISI YA BUNGE)
No comments:
Post a Comment