HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 25, 2018

Dot TZ registry (TZNIC) yadhamini mkutano wa ICT Arusha

Mhandisi wa Mifumo ya dot TZ kutoka Tanzania Network Information Centre (TZNIC), Bw. Raymond Linus akiongea na wataalamu wa ICT na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa kuwa na kikoa cha .tz (.tz domain name) katika mkutano wa ICT uliofanyika Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA). Dot TZ registry imekua ikidhamini mikutano hii ya ICT kuelimisha wananchi juu ya faida ya kutumia kikoa cha .tz katika mawasiliano ya Intaneti.
Mkuu wa Idara ya Informatics wa Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA) Bi. Pamela Chogo akiwakaribisha wataalamu na wanafunzi wa ICT kwenye mkutano wa ICT uliofanyika Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA) Dr. Samwel Werema akizungumza na wanafunzi wa ICT kwenye mkutano wa ICT uliofanyika Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA).
Wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha walioshiriki mashindano ya ICT (Arusha ICT Innovative Challenge 2018 – Jiji Hackathon) wakiwa kwenye picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad