Wakazi wa Kinondoni Mahakamani wamelalakia maji yaliyozingira nyumba zao kutokana na baadhi ya wakazi hao kujenga katika mkondo wa maji.
Akizungumza leo mkazi wa eneo Bi. Khadija Hamis amesema kutokana na mvua za masika zinazoendelea kunyesha wanapata adha ya maji hayo yanayotuama kwenye eneo hilo.
Amesema kuwa baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamezingirwa na maji kwa wiki mbili na hakuna chochote kinachofanyika.
Aidha amesema kutokana na hali hii kuendelea wanaiomba serikali kutatua tatizo hili mara baada ya kuisha masika.
Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali katika jiji la Dar es Salaam iliyoanza kunyesha wiki iliyopita, zimesababisha maafa, uharibifu wa miundombinu ya baarabara pamoja na baadhi nyumba katika eneo la Kinondoni Mahakamani kuzungukwa na maji ya mvua jijini Dar es Salaam.
Mwanafunzi akikwepa dimbwi la maji machafu ya mvua kama yanavyoonekana pichani leo jijini Dar es Salaam.picha zote na Emmauel Massaka,Globu ya jamii.
No comments:
Post a Comment