HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 16, 2017

MWILI WA MAREHEMU AMINA ATHUMAN KUWASILI JIJINI DAR ASUBUHI HII NA BAADAE KUSAFIRISHWA KIJIJINI KWAO LUSHOTO KWA MAZISHI

  Mwili wa mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la uhuru na mzalendo Amina Athuman ukisafirishwa asubuhi hii na boti ya kilimanjaro kuelekea Dar es Salaam na kusafirishwa hadi kijijini kwao Lushoto kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika siku ya jumanne mchana. Marehemu alikuwa Zanzibar kikazi akiripoti habari za michezo kombe la Mapinduzi na kumkuta mauti hayo baada ya kujifungua mtoto wa kiume, kwa bahati mbaya mtoto akafariki baada ya kuzaliwa na yeye kupata kifafa cha uzazi na kufariki jana asubuhi. Mwenyenzi mungu ampe kauli thabiti na amsamehe madhambi yake-Ameen

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad