HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 11, 2017

MKUU WA MKOA WA MBEYA AINGILIA KATI MGOGORO WA HALMASHAURI YA MBEYA NA WAFANYABIASHARA SOKO LA MBALIZI ...

Image may contain: 8 people, people smiling, crowd and outdoor
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla aagiza vyumba vya wafanyabiashara vilivyofungwa na halmashauri vifunguliwe mara moja,
awarejesha wafanyabiashara kwenye meza ya mazungumzo na kuiondoa kesi baraza Ardhi , Ampa mkurugenzi siku 7 amalize Mgogoro wa KODI na wafanyabiashara kwa kukaa meza moja na wafanyabiashara.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla  amefanya ziara katika mji wa Mbalizi kwa kutembelea stendi na soko la mbalizi na baadaye kufanya mkutano wa hadhara na wafanyabiashara na wananchi wa mji wa mbalizi
Baada ya kusikiliza  kero za wafanyabiashara na wananchi amemwagiza mkurugenzi na baraza la madiwani kukaa Ndani ya siku saba kumaliza mvutano wa kodi ya pango ya vyumba sokoni.
Amesikitishwa kwa namna ambavyo Mgogoro huo umeachwa muda mrefu bila kushughulikiwa na kusababisha mvutano na halmashauri kushtakiwa baraza la Ardhi
Ameagiza uongozi wa halmashauri na Mamlaka ya mji Mdogo wa Mbalizi kusimamia usafi.
Wananchi na wafanyabiashara wameshukuru na kupongeza uamuzi wa Mkuu wa Mkoa na wamehaidi ukitoa kesi mahakamani na kukaa ktk meza ya mazungumzo na halmashauri kumaliza mvutano wa pango la vibanda vya biashara
Image may contain: 15 people, people standing and outdoor
Image may contain: 1 person, standing, outdoor and indoor
Baadhi ya wakazi na wafanyabishara wa soko la Mbalizi wakitoa kero zao kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya alipo fanya ziara katika Stendi ya Mabasi na Soko la Mbalizi Mkoani Mbeya.
Image may contain: 2 people, people standing
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara na wafanyabishara na wananchi wa Mji mdogo wa Mbalizi Mkoani Mbeya.
Image may contain: 11 people, people standing

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad