Kamanda wa Kanda maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akizungumza na waandishi wa waandishi leo wa habari ofisi kwake makao makuu Kanda maalum ya Dar es Salaam.
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Jeshi la Polisi mkoa wa Dar es Salaam limekamata watuhumiwa 22 hatari wa makosa ya wizi kwenye taa za Chang’ombe na kungwineko jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Kamanda wa Kanda maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema kuwa kikosi maalum cha kupambana na wizi wa kutumia silaha na wizi wa nguvu cha Polisi Kanda maalum DSM kimefanikiwa kuwakamata watuhumiwa hatari 22.
“ufuatiliaji ulifanyika ka kuwakamata watuhumiwa hao kwa nyakati tofauti kama ifuatavyo mnamo tarehe 11.12.2016 huko Temeke maeneo ya Keko Magurumbasi na mataa ya VETA Chang’ombe askari walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa 10 kwa makosa ya wizi kutoka maungoni na wizi kutoka kwenye magari” amesema Kamanda Sirro.
Amesema kuwa wakati huohuo jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam kupitia kikosi chake cha kupambana na wizi wa magari kimefanikiwa kukamata magari matatu katika mikoa mbalimbali kama ifuatavyo
1.gari Toyota T386 CGY aina ya Verosa rangi nyeusi mali ya Abraham Robert wa jijini Dar es Salaam ambapo gari hili lilikamatwa Mbeya likiwa limetelekezwa.
2.Gari Toyota T946DGH aina ya IST rangi ya fedha ikiwa imeendeshwa na mtuhumiwa aitwaye Hamad Said ,miaka 27 mkazi wa Kimara Dar es Salaam ambapo gari hiyo ilikamatwa mkoani Morogoro,gari hiyo iliibiwa maeneo ya Kawe beach .
No comments:
Post a Comment