Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
BAADA ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kuamrisha klabu za Yanga na Simba kufanya mabadiliko ya katiba hatimaye Uongozi wa klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba wameitisha mkutano mkuu wa dharula unaotarajiwa kufanyika Desemba 11 mwaka huu.
mkutano huo wa dharula umeitishwa ikiwa ni katika mchakato wa kuingia kwenye mfumo mpya wa mabadiliko ya uendeshaji wa klabu hiyo utahusihsa moja kwa moja kubadili katiba yao.
Mkuu wa kitengo cha habari wa Simba, Haji Manara ametoa taarifa hiyo leo na kuweka wazi kengo la kufanya mkutano wa dharula ukiwa mlengo thabiti wa kufanya mabadiliko ya katiba ili kuweza kwenda mchakato mpya wa uendeshaji wa klabu hiyo.
Barua hiyo rasmi iliyotolewa leo na Uongozi wa Simba baada ya kamati ya utendaji ikiongozwa na Rais Evance Aveva walikubaliana kuitisha mkutano mkuu wa dharula kwa mamlaka ya katiba yao inayowaruhusu ya ibara ya 22 kifungu cha kwanza na nyaraka zote za ajenda ya mkutano huo zitakabidhiwa kwa matawi kama ibara ya 22 kifungu cha nne kinavyosema.
No comments:
Post a Comment