HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, July 31, 2016

WAOGELEAJI WAWILI KUIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI NCHINI BRAZIL

Magdalena Mosha akiwa pamoja na mshiriki mwenzie Hilal Hilal wakiwa kwenye mazoezi ya mwisho kabla ya kuondoka kuelekea nchini Brazil. 
Na Zainab Nyamka.

WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya Olimpiki inayotarajiwa kufanyika katika mji wa Sao Paulo, Rio De Jeneiro nchini Brazil , timu ya kuogelea imefanya mazoezi yake ya mwisho kabla ya kukabidhiwa bendera na Kamati ya Olimpiki nchini TOC kwa ajili ya kuiwakilisha vyema katika mashindano hayo.

Timu hiyo itakayowakilishwa na waogeleaji wawili ambao ni Magdalena Moshi anayeenda kwa mara ya tatu kwa upande wa wanawake huku Hilal Hilal akienda kwa mara ya kwanza na wote watakuwa ni waogeleaji katika upande wa mita 50. Akizungumzia maandalizi ya mwisho Kocha wa timu hiyo Alexandra Mwaipasi amesema kuwa wachezaji wake wameiva kwani mwanzoni walikuwa na changamoto ya kupata mabwawa yenye viwango vinavyoendana na mashindano hayo ila kwa mwaka huu washiriki wote wameweza kuweka kambi katika nchi mbili tofauti ambapo Magdalena amekuwa Australia huku Hilal akijifua nchini Dubai.

Amesema, ana imani na wachezaji wake kwani kwa kipindi alichokaa nao ameona uwezo waliokuwa nao na  wanaweza kurudi na medal nyumbani. Naye Katibu mkuu wa chama cha kuogelea TSA Ramadhan Namkoveka amesema kuwa tofauti na wengine wao hawajapata wadhamini ila wachezaji wao wamejiandaa vizuri na wana imani kubwa kuwa wataweka historia.

Moja ya washiriki, Magdalena Mosha amesema kuwa amejiandaa vizuri na anaamini miaka aliyoshiriki kwenye mashindano ya Olimpiki ya Beijing na London yamempa uelewa zaidi wa nini anatakiwa kufanya mwaka huu na katika mazoezi yake nchini Australia  ameyafanyia kazi. Amesema kuwa kwa sasa macho ya watanzania yapo kwao na wanatoa ahadi ya kufanya vizuri kwani hata mshiriki mwenzie  Hilal amekuwa kwenye mazoezi mazuri nchini Dubai tena katika kituo kinachojihusisha na masuala ya uogeleaji.

Timu hiyo kesho inakabidhiwa bendera na TOC kabla ya Agosti 02 kuondoka kuelekea nchini Brazili.
Magdalena na Hilal wakiwa katika mazoezi ya mwisho.
Viongozi wa Chama cha Kuogelea TSA wakiwa pamoja na washiriki Hilal Hilal na Magdalena Mosha, Kushoto ni mkurugenzi wa ufundi Amina Mfaume, Mwenyekiti wa TSA Alex Mosha, Katikati ni Kocha wa timu ya kuogelea Alexandra Mwaipasi na mwisho kulia ni Katibu mkuu TSA Ramadhan Namkoveka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad