
Wakufunzi kutoka Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani(KMKGM) wakionesha onesho la kijasiri kama inavyoonekana katika picha.



Mgeni rasmi akimkabidhi cheti cha sifa mmoja wa Askari Wahitimu ambaye amefanya vizuri zaidi katika nyanja ya Nidhamu katika kipindi chote cha Mafunzo hayo.


Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa karibu Maonesho mbalimbali katika Uwanja wa Gwaride kwenye hafla ya kufunga Mafunzo hayo.

Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP - John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kutoa hotuba yake ya kufunga rasmi kwa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza katika Chuo cha Magereza, Kiwira Mbeya.

Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP - John Casmir Minja(wa pili kulia)akiwa ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi(wa pili kushoto) mara baada ya sherehe za kufunga Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza, Chuo cha Magereza, Kiwira Mbeya(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza - Kiwira, SACP. Stanford Ntirundura(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:
Post a Comment