HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 4, 2016

KINONDONI:WATENDAJI WA KATA WAWILI WAFUKUZWA KAZI.

 Meya wa Halmashauri ya Manispaa Kinondoni  Boniface Jacob  akizungumza na  Mafisa Watendaji  juu ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni  na kuwafukuza kazi mafisa watendaji kata wawili kutokana ubadhirifu fedha za umma.
(Picha na Emmanuel Masaka,Globu ya Jamii.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
HALMASHAURI ya Manispaa ya kinondoni imefukuza kazi mafisa watendaji kata wawili kutokana ubadhirifu fedha za umma.

Akizungumza leo na maafisa watendaji kata, meya wa kinondoni boniface jacob amesema kuwa hawatavumilia  watendaji wanaofuja fedha za umma.

Watendaji waliofukuzwa ni Ernest Misa na Ally Bwanamkuu na wengine wawili wamesimamishwa kazi kwa uchunguzi ambao ni Shaban Kambi pamoja na Bernard Supu. 

Aidha Meya huyo amesema zipo kata tano ambazo zimekusanya mapato vizuri na kata tano zingine zimefanya vibaya hivyo wanatafuta dawa ya kuwaondoa watendaji waliofanya vibaya.

Jacob amesema migogoro ya ardhi imepungua kutokana na kila watendaji kuwajibika katika zao awali migogoro ilikuwa inasababishwa na wenyewe

Amesema kinondoni wanataka kuibadili katika kuhakikisha watendaji wanawahudumia wananchi kuachana kufanya kwa mazoea.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad