HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 19, 2016

TFF TUNAOMBA FAINALI FA ISOGEZWE MBELE - YANGA

Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KLABU ya Yanga imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kusogeza mbele fainali ya kombe la Shirikisho FA, kwakuwa ratiba ya ligi kuu kuoneana kuwabana.

Awali fainali hiyo ilipangwa kufanyika Juni 11 lakini jana TFF ilibadilisha tarehe hiyo na kusema àassaaaqàa 25 ndiyo itapigwa faainali.

Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano amesema  wanawaomba TFF kusogeza mbele ratiba hiyo kwani ratiba imewabana hasa ukilinganisha kuwa kikosi chao bado hakijarea na kitakaporejea kitapumzika masaa machache kisha kitaanza safari ya kuelekea Songea kwa usafiri wa gari ambapo masaa zaidi ya 14 watakuwa njiani na watashuka dimbani Jumapili na Jumatatu wataanza safari ya kurudi Dar es salaam.

"Ukiangalia ratiba inabana huwezi kurudi Jumatatu usiku halafu Jumatano tuingie uwanjani kwa ajili ya kombe la FA ambao ni moja ya mchezo muhimu kwetu," amesema. Kwahiyo kwa heshima wanaomba wafikiriwe katika hilo kwani kwakuwa wachezaji watajumuika na timu zao za Taifa basi fainali hiyo inaweza kusogezwa ikasubiri mechi za kitaifa kumalizika.

Kutokana na hilo Yanga wametaka waweze kufikiriwa kulingana na ratiba ilivyo pamoja na hilo serikali inatakiwa kushirikiana na TFF kuweza kuzisaidia klabu pale zinapoenda nje ya nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad