HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 10, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA RASMI JENGO LA KITEGA UCHUMI LA NSSF JIJINI ARUSHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mipango (kulia kwake), Waziri wa Kazi wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge kazi ajira na vijana Jenista Mhagama (kushoto kwake), Meya wa Jiji la Arusha,mstahiki Calist Lazaro Bukhai (kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof. Godius Kahyarara (wa pili kushoto) na viongozi wengine mbali mbali kwa pamoja wakita utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo la kitega uchumi la NSSF Mafao House jijini Arusha Mei, 9 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Kazi wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge kazi ajira na vijana Jenista Mhagama, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mipango wakivuta pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo la kitega uchumi la NSSF Mafao House jijini Arusha Mei, 9 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo ya mradi wa ujenzi wa Jengo la kitega uchumi la NSSF Mafao House, kutoka kwa Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi John Msemo, jijini Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia wakati kikundi cha ngoma za asili cha kimasai kilipokuwa kikitumbuiza pembezoni mwa jengo la kitega uchumi la NSSF jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad