HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, April 9, 2016

TRA YAENDELEZA ZOEZI LA KUBOMOA MTANDAO WA WAFANYA BIASHARA YA MAGENDO UKANDA WA KUSINI MWA PWANI

Na Mwandishi Wetu-Kilwa

Siku ya tarehe 6/4/2016 maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kikosi cha (FAST) wakiwa na maofisa wa Polisi walifanya upekuzi kwa lengo la kutafuta magendo kwenye nyumba ya mfanyabiashara Yusuf Barkat Sareh, iliyopo
Somanga njia nne eneo la Kikanda Wilaya ya Kilwa mkoa wa Lindi na kubaini kuwepo kwa bidhaa nyingi za magendo.

Upekuzi huo ulifanyika baada ya kupata taarifa za kiintelijensia zilizofanyiwa kazi muda kwa haraka na kubaini kupowe kwa Bidhaa mbalimbali kutoka nje ya nchi zilikutwa kwenye baadhi ya majengo, ambazo ni Sukari ya India kilo 50 jumla mifuko 762, Sukari ya nje iliyokamatwa kwenye mifuko ya viwanda vya hapa nchini kilo 25 jumla mifuko 135, Mafuta ya kula lita ishirini (20) aina mbalimbali kutoka nje jumla madumu 49, Betri aina ya tigger katoni 223, Amira katoni 135, Sabuni za kufulia katoni 48

Vitu mbalimbali vilivyokamatwa kama ushahidi wa biashara haramu ya magendo ya sukari ni Mashine mbili (2) za kushonea kwenye mifuko iliyowekwa sukari inayotoka nje ya nchi na kuwekwa kwenye mifuko ya viwanda vya nchini nya sukari vya Kilombero,TPC na Mtibwa Sugar, Mifuko mitupu mipya ya sukari kilo 25 toka India 2000, Mifuko iliyotumika ya kilo 50 mitupu ya sukari 36,000, Mifuko ya sukari iliyotumika ya Viwanda vya Tanzania ya kilo 25 kiasi cha 1150, Madumu ya mafuta ya nje mchanganyiko ya kula lita 20 kiasi cha 609, Madumu matupu ya lita 10 ya nje kiasi cha 310.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Richard Kayomboakionesha ndoo zinazotarajiwa kuwekwa mafuta.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Richard Kayombo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA akionesha sukari.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Richard Kayombo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA
Sukari na viroba vya kuweka kwa matayarisho ya kuingizwa sokoni.
Hii ni Sukari iliyomwangwa chini kabla ya kuwekwa kwenye viroba
Askari wakisimamia zoezi la kuvunja mlango



Nyumba hii ndiyo Ofisi ya Bosi ambayo utumika kuweka bidhaa kabla ya kusambazwa sokoni iliyopo Somanga njia nne eneo la Kikanda Wilaya ya Kilwa mkoa wa Lindi.
sehemu ya kuweka sukari na kupima.
Nyumba inayotumika kuweka sukari
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Richard Kayombo akizungumza na waandishi.
 
Aina ya mafuta kutoka nje ya nchi tayari kuwekwa kwenye ndoo kwa kupeleka Sokoni
Polisi akilinda viroba vyenye sukari kutoka nje ya nchi.
Madumu yaliyokua na mafuta ya kula na ndoo zinazotarajiwa kuwekwa mafuta
Nyumba ya mtuhumiwa Yusuf Sareh iliyopo Somanga Njia nne Kikanda.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad