HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 11, 2016

TAASISI YA BASILLA MWANUKUZI YAZINDULIWA RASMI LEO JIJINI DAR

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (wa pili kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Taasisi ya Basila Mwanukuzi (Basila Mwanukuzi Empowerment Foundation) yenye lengo la kusaidia wanawake kuinua uwezo wao wa kibunifu ili kujiinua kiuchumi  hasa Mama Lishe kwa kushirikiana na wadau mbali mbali. Uzinduzi huo umefakika leo Aprili 11, 2016 kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Mwanzilishi wa Taasisi hiyo, Basila Mwanukuzi (kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jinsia, Timoth Mgonja pamoja na Mwakilishi wa Mama Lishe, Bi. Grace Foya.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu, akitoa hotuba yake wakati wa Uzinduzi wa Taasisi ya Basila Mwanukuzi (Basila Mwanukuzi Empowerment Foundation), uliofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es salaam leo Aprili 11, 2016.
 Mwanzilishi wa Taasisi ya Basila Mwanukuzi (Basila Mwanukuzi Empowerment Foundation), Basila Manukuzi, akizungumza machache wakati wa hafla ya uzinduzi wa Taasisi yake hiyo yenye lengo la kusaidia wanawake kuinua uwezo wao wa kibunifu ili kujiinua kiuchumi  hasa Mama Lishe uliofakika leo Aprili 11, 2016 kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es salaam
Familia ya Basila Mwanukuzi, wakifatilia hafla hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa kutoma sehemu mbali mbali.
Baadhi ya wakina Mama Lishe kutoka Wilaya za Ilala na Kinondoni wakiwa kwenye hafla hiyo.

Wadau.
  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu, akisalimiana na Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waandaaji wa Mashindano ya Miss Tanzania, Anko Hashim Lundenga wakati walipokutana kwenye hafla hiyo.
Picha ya pamoja na baadhi wa Wageni wa waalikwa pamoja na Kina Mama Lishe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad