HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, April 3, 2016

Sh1.5 bilioni kujenga kipande cha barabara ya mbozi, Temeke

Mansipaa ya Temeke imetenga kiasi cha sh bilioni 1.5 kwa mwaka huu wa fedha wa 2016/2017 kwa ajili ya ujenzi, kiwango cha lami kipande cha barabara ya Mbozi chenye urefu wa kilometa 1.3 kinachopiota nje ya Kiwanda cha Mabati cha Alluminium Africa (ALAF).

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi leo (jumapili), mkurugenzi wa manispaa ya Temeke, Photidas Kagimbo alisema manispaa yake imetenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya ujenzi wa kipande hicho cha barabara chenye urefu wa kilometa 1.3.

Alisema ujenzi huo utafanyika baada ya malalamiko ya muda mrefu ya wafanyabiashara wa eneo hilo wakiwemo wamiliki wa viwanda ambako barabara hiyo inapita ikiunganisha ile ya Mbozi hadi barabara ya Nyerere, jirani na Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD).

Alisema awali walifanya mazungumzo na kiwanda cha ALAF na Steel Masters ili kuangalia jinsi ya kutatua changamoto hiyo na baada ya ufuatiliaji wa muda mrefu hatimaye hivi sasa itajengwa ifikapo mwaka mpya wa fedha 2016/2017.

“Ni changamoto ya muda mrefu lakini sasa imepata ufumbuzi” alisema na kuongeza kuwa awali ilikuwa inajengwa ili iweze kupitika lakini kutokana na shehena za mizigo mizito zinazopitishwa katika barabara hiyo uhai wake unakuwa wakati wa kiangazi na mvua zikinyesha kunakuwa na mashimo makubwa.
Alisema magari yenye mizigo mizito ambayo mengine ni hadi tano 40 ni changamoto kwa barabara hiyo lakini hata hivyo sasa inajengwa kiwango cha lami hivyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuwapunguzia adha wenye viwanda na pia wafanyabiashara wa soko la Mapambano.

Awali wakizungumza kwa nyakati tofauti na mandishi wa habari hizi, wafanyabiashara katika soko hilo la Mapambano walidai kuwa wanapata shida hususan siku za mvua kwani magari yamekuwa hayapiti barabara hiyo zaidi ya yale ya mizigo mikubwa.

“Wateja wetu ambao wanatumia magari madogo au yale yenye uzito uziozidi tani tatu na nusu hawawezi kutufikia na mbaya zaidi hata sisi wenyewe wakati mwingine tunashindwa kufika katika fremu zetu” alisema Grace Sanga.

Katibu wa Jumuia ya Vikundi vya Wenyeviwanda na Biashara Ndogondogo (Vibindo), wilaya ya Temeke Paul Luanda alikiri kuwepo kwa adha hiyo ambayo inawakwamisha kibiashara hususan nyakati za mvua.

“Hata hivyo manispaa Temeke inatupa ushirikiano kwani hivi karibuni ilitoa mabomba kwa ajili ya kutusaidia kuondoa maji ili magari yaweze kutufikia na sisi kufanyabiashara” alisema na kuongeza kuwa mashimo makubwa yanafanya magari madogo kushindwa kupita eneo hilo hivyo wao kukosa biashara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad