HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, April 9, 2016

MWANAMUZIKI NDANDA KOSOVO AFARIKI DUNIA LEO

Mwanamuziki mkongwe aliyewahi kujizolea sifa kem kem katika miondoko ya dansi hapa  nchini wakati akiwa na bendi ya FM miaka ya nyuma kabla ya kujiengua na kuunda kundi lake lililojulikana kwa jina la Stono Musica a.k.a Wajela Jela Gwaa, Ndanda Kosovo ‘Kichaa’ amefariki Dunia leo asubuhi,baada ya kuugua kwa siku chache

Taarifa kutoka kwa mtu wake wa Karibu ambaye pia ni Mwanamuziki wa dansi, Kardinal Gento amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na ameongeza kuwa Ndanda Kosovo amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa tangu juzi kutokana na matatizo ya tumbo.

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi-AMIN.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad