Na Editha Karlo wa Globu ya Jamii, Kigoma.
WAZIRI
Mkuu, Kassim Majaliwa amemtaka Mkurugenzi wa manispaa ya Kigoma Ujiji,
Mhandisi na Mhasibu kupeleka taarifa ya maandishi kwa katibu tawala wa
mkoa juu ubadhirifu waliofanya wa mali za umma.
Hayo
ameyasema leo wakati akiongea na watumishi wa Wilaya zote kwenye kikao
cha majumuisho ya ziara yake kilichofanyika katika ukumbi wa NSSF .
Alisema
kuwa katika halmashauri ya Kigoma Ujijikuna ubadhirifu wa malu za umma
umefanyika wa kuuza soki la Kigodeko,jengo la baby come na jengo la mi
boss kwa kiasi cha shilingi milioni mia tatu badala ya milioni 800.
Alisema
kuwa anawataka wajieleze kwa katibu tawala wa Mkoa kea maandishi ni
utaratibu upi wametumia kuuza mali za umma na kwanini walikiuka agizo la
mkuu wa Mkoa la kuwataka wasiuze mali hizo.
Majaliwa
alisema kuwa maelezo yao anayataka jumamosi ya tarehe mbili
yaweyamekamilika na kufika ofisini kwakwe ili kama kuna ukweli hatua za
kinidhamu ziwe kuchukuliwa kwa waliohudika na ubadhilifu huo.
Akiongea
na mtandao huu juu ya tubuma hizo mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma
Ujiji mhandisi Boniface Nyembele alisema kuwa ni kweli mali hizo wameuza
lakini kwa kufuata utaratibu.
"Utaratibu
wote tulifuata kuuza malu hizo na vikao halalu vilikaa na kupitisha na
mihutasari ya vikao ipi na tenda tulitangaza tika mwaka 2013 tumeuza
mwaka huu mwezi wa 6"alisema Mkurugenzi
Alisema fedha walizouza zilitumika katika ujenzi wa mahabara na shughuli zingine.
'Kwakuwa waziri mkuu ametutaka tujieleze kwa maandishikwa katibu tawala turafanya hivo kwani kila kitu kipo wazi"alisema.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongea na watumishi kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Kigoma juu ya ziara yake ya kikazi Mkoani hapa.
Baadhi ya watumishi na viongozi wa mkoa wa Kigoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majliwa katika Kikao cha Majumuisho ya ziara yake mkoani humo kwenye ukumbi wa NSSF Desemba 30, 2015.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongea na watumishi kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Kigoma juu ya ziara yake ya kikazi Mkoani hapa.
Baadhi ya watumishi na viongozi wa mkoa wa Kigoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majliwa katika Kikao cha Majumuisho ya ziara yake mkoani humo kwenye ukumbi wa NSSF Desemba 30, 2015.
No comments:
Post a Comment