HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, November 7, 2015

Boko Beach Veterans wamkabidhi zawadi Mchezaji bora wa Mwezi Oktoba 2015

Mwenyekiti wa Timu ya Boko Beach Veterans (BBV), Danny Ole a.k.a Aguero (wa nne toka kushoto) akimkabidhi zawadi ya mpira Mchezaji bora wa Mwezi Oktoba, Henry Horombe (wa nne toka kulia), baada ya kuonyesha kiwango kizuri kwa kipindi chote cha mwezi mwezi huo 2015. Zawadi hizo hutolewa na mdau mkubwa wa soka nchini na mmiliki wa maduka ya Zizzou Fashion, Othman Tippo Shaaban ambaye nae ni mwanachama wa timu hiyo.
Sehemu ya wachezaji wa Timu ya Boko Beach Veterans (BBV) wakimpongeza mchezaji mwanzao aliebuka kidedea na kutwaa taji la Mchezaji bora wa Mwezi Oktoba, Henry Horombe (katikati) mara baada ya mtanange uliopigwa mapema leo asubuhu katika uwanja wa Boko.
 Timu ya Boko Beach Veterans (BBV) ikiwa imegawanyika katika mchezo wa mazoezi mapema leo asubuhi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad