HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 24, 2014

TMK FAMILY na Mkubwa na Wanawe Yamoto Band watoa Msaada katika wodi ya watoto Hospitali ya Temeke

 Timu nzima ya TMK Family na Mkubwa na Wanawe Yamoyo Band chini ya uongozi wake Said Fella (mwenye shati la draft) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati walipofika kwenye Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam,kwa lengo la kutoa Msaada wa bidhaa mbali mbali wa watoto wanaotibiwa katika Hospitali hiyo.TMK Family na Mkubwa na Wanawe Yamoyo Band walifanya hivyo ikiwa ni sehemu ya kugawana kile kidogo wanachokipata na jamii inayowazunguka.
 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,Mh. Temba akiwa amebeba moja ya mabox ya bidhaa walizozikabidhi hospitalini hapo.
 Kiongozi wa Bendi iliyochipukia hivi karibuni na kufanya vyema katika tasnia ya muzini ifahamikayo kama Yamoto Band,Dogo Asley nae hakuwa nyuma katika zoezi hilo.
 Mh. Temba na mtoto akimpatia mmoja wa watoto waliolazwa hospitalini hako moja ya bidhaa walizokuwa nazo.
 Msanii Chegge pia akifanya hivyo.
 Kiongozi wa TMK Family na Mkubwa na Wanawe Yamoyo Band,Mkubwa Said Fella akikabidhi sehemu ya misaada hiyo kwa Wauguzi wa Hospitali ya Temeke ikiwa ni mchango wao kwa Jamii inayowazunguka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad