HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, June 20, 2014

Mbuzi wa Morogoro ni noma sana,wanauwezo wa kipekee sana wa kula majani

Siku moja katika pita pita za Mdau Juma Mtanda,alikatiza barabara ya Sabasaba Mkoani Morogoro na kufanikiwa kuzinasa taswira hizi za Mbuzi wakila majani katikati ya barabara na kusababisha magari na vyombo vingine vinavyotumia barabara hiyo vikiwa na upole usiotegemewa kama inavyoonekana pichani hapa.kwa mujibu wa baadhi ya wapita njia hiyo wameeleza kwamba mbuzi hao wenye uwezo wa kipekee wa ulaji wa majani katikati ya lami ambao wako makundi kwa makundi,pamoja na kwamba halmashauri ya Manispaa hiyo ya Morogoro imeipiga mikwara mifugo hiyo pamoja na wamiliki wake,lakini wenyewe hawajali wala nini na ndio kwaanza wanaendelea kupiga misele.
Mbuzi hawa hawaogopi cha nini wala nini,si unaona hapa jinsi walivyoizunguka hii baiskeli.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad