Timu
nne za soka za kanda ya mashariki zimefanikiwa kuvuka na kutinga hatua
ya ligi ndogo ya mashindano ya Castle Lager Perfect Six kwa mikoa ya
Morogoro na Dodoma.
Katika
michezo ya hatua ya mchujo ikirishikisha timu nane za mikoa hiyo, kwa
upande wa Morogoro timu za Mzinga FC na Ndezi FC zenyewe zilikata mapema
tiketi ya kucheza ligi hiyo huku kwa Dodoma ikiwa ni Schalke 04 FC
pamoja na Market FC.
Schalke
04 na Market FC zilikata tiketi juzi kwa kushika nafasi ya kwanza na
pili katika uwanja wa Central msikiti wa Gadaff mjini Dodoma baada ya
kuvuka katika hatua ya mchujo wakati Ndezi FC na Mzinga FC zikifanya
hivyo katika michezo iliyofanyika uwanja wa shule ya msingi Kiwanja cha
Ndege Manispaa ya Morogoro.
Meneja
wa Bia ya Castle Lager, Kabula Nshimo waandaaji wa Castle Lager Perfect
Six alisema kuwa baada ya kumalizika kwa hatua ya mchujo kwa michezo
iliyofanyika Morogoro na Dodoma inayounda kanda ya mashariki na kupata
timu nne, timu hizo zitacheza ligi ndogo ili kupata timu moja
itayowakilisha kanda ya mashariki katika mashindano hayo ya taifa jijini
Dar es Salaam.
Nshimo
alisema kuwa ligi ndogo itafanyika Juni 7 mwaka huu Manispaa ya
Morogoro kwa kuzikutanisha washindi wa kwanza wa Dodoma ambazo ni timu
za Schalke 04 na Market FC na Ndezi FC na Mzinga FC ili kucheza na
kupata mshindi wa kanda ya mashariki atayewakilisha kanda hiyo kwenye
mashandano hayo jijini Dar es Salaam.
Alisema
shindano la Castle Perfect Six limelenga kuzungumza na wanywaji wa
Castle Lager ambao wana shauku ya kucheza mpira wa miguu na kujumuika
pamoja.
Nshimo
alisema kuwa mechi zilizochezwa wikendi hii zimeonyesha jinsi gani
Watanzania wana mwamko na shauku kubwa ya kushiriki mashindano kutokana
na watu kujitokeza kwa wingi maeneo mbalimbali ambapo yalifanyika
mashindano hayo ya kwanza.
Vilevile
wikendi hii yalifanyika mashindano hayo kwenye mkoa wa Dar es salaam
kwenye viwanja vya Barafu Mburahati, uwanja wa Garden uliopo Kinondoni,
Bulyaga Temeke katika hatua za awali za kupata wawakilishi wa Kanda hiyo
watakaocheza fainali za taifa. Mashindano yanaendelea pia kwenye mikoa
ya Mwanza na Musoma katika hatua ya mwanzo kupata wawakilishi wa kanda
ya Ziwa.
Mechi
zilizochezwa wikendi hii ilikuwa ni awamu ya kwanza ya mashindano hayo
ambapo timu zitakazofuzu hatua hiyo ya mikoa zitachuana katika ngazi ya
kanda na hatimaye taifa. Washindi wa fainali za taifa watajipatia fursa
ya kipekee kwenda kutembelea jiji la Barcelona huko Hispania na kuiona
timu ya Barcelona ikicheza na pia wataweza kujionea mambo mbalimbali ya
kihistoria katika uwanja wa Camp Nou.
Mchezaji
wa timu ya Matema,Hafidh Mohammed (kulia) akipiga hesabu za kumtoka
mchezaji wa IP Sports Club, Hamis Daudi katika mashindano ya Castle
Lager Perfect Six kwenye viwanja vya Garden Kinondoni jijini Dar es
Salaam jana.Matema ilishinda 2-0.
Mchezaji
wa timu ya IP Sports Club,Hassan Chidigo (kushoto) akijaribu kufunga
katika gori la Matema,katika mashindano ya Perfect Six kwenye viwanja
vya Garden kinondoni jijini Dar es Salaam jana.Matema ilishinda 2-0.
Kipa
wa timu ya Matema,Wahabi Mkambe (kulia) akimpiga chenga mchezaji wa IP
Sports Club,Jaffary Madega katika mashindano ya Castle Lager Perfect Six
kwenye viwanja vya Garden Kinondoni jijini Dar es Salaam jana.Matema
ilishinda 2-0.
Mchezaji
wa timu ya Matema,Hafidh Mohammed (kulia) akipiga chenga mchezaji wa IP
Sports Club,Hamis Daudi katika mashindano ya Castle Lager Perfect Six
kwenye viwanja vya Garden kinondoni jijini Dar es Salaam jana.Matema
ilishinda 2-0.
Mchezaji
wa Timu ya, Pile FC, Ukwama Bonny katikati akiwatoka wachezaji wa timu
ya Mwangaza, wakati wa Mchezo wa Fainali katika Bonanza Castle Lager
Perfect Six uliofanyika kwenye Uwania wa Buliyaga Temeke Dar es Salaam
ilishinda kwa penati, 6. 5.
Kipa
wa timu ya Rafael Abuu Mauri (kushoto) akijaribu kumtoka mchezaji wa
Saigon, Ally Said zote za Mburahati katika bonanza la ‘Castle Lager
Perfect Six’ lililofanyika mwishoni mwa wiki katika kiwanja, Mburahati
jijini Dar es Salaam ambapo kwa washindi wa jumla watapata fursa ya
kwenda katika jiji la Barcelona, Hispania kuishuhudia timu ya Barcelona.
Saigon ilishinda 4-1.
Mchezaji
wa timu Saigon, Habib Iman akijaribu kumfunga kipa wa timu ya Rafael
Abuu Mauri zote za Mburahati katika bonanza la Castle Parfect Six
lililofanyika mwishoni mwa wiki katika kiwanja, Mburahati jijini Dar es
Salaam ambapo kwa washindi wa jumla watapata fursa ya kwenda katika jiji
la Barcelona, Hispania kuishuhudia timu ya Barcelona. Saigon ilishinda
4-1.
Wachezaji
wa timu ya Rafael, Habib Iman (kushoto) na Omary Nchimbi wa Sigon zote
za Mburahati wakikabana katika bonanza la Castle Lager Perfect Six
lililofanyika mwishoni mwa wiki katika kiwanja, Mburahati jijini Dar es
Salaam ambapo kwa washindi wa jumla watapata fursa ya kwenda katika jiji
la Barcelona, Hispania kuishuhudia timu ya Barcelona. Saigon ilishinda
4-1.
Mchezaji
wa timu ya Barcelona, Ally Rajabu (kushoto) akijaribu kumtoka mchezaji
wa Saigon, Ally Said zote za Mburahati katika bonanza la Castle Lager
Perfect Six lililofanyika mwishoni mwa wiki katika kiwanja, Mburahati
jijini Dar es Salaam ambapo kwa washindi wa jumla watapata fursa ya
kwenda katika jiji la Barcelona, Hispania kuishuhudia timu ya Barcelona.
Saigon ilishinda 3-1.
Mchezaji
wa timu ya Market FC, Kamal Omary akichuana Mgaya Daud wa timu ya
Kisimpite FC kushoto wakati wa michezo ya kusaka timu mbili za mkoa wa
Dodoma zitazoshindana na nyingine mbili za Morogoro ili kucheza ligi
ndogo na kupata timu moja itayowakilisha mashindano ya Castle Lager
Perfect Six kutoka kanda ya katika michezo iliyofanyika kwenye uwanja wa
Centel mjini Dodoma juzi ambapo katika mchezo Martet FC ilishinda bao
2-1.
Mchezaji
wa timu ya Market FC, Medi Mwanyemba kushoto akizongwa na mchezaji wa
Kisimpite Mgaya Daud kulia wa timu ya Kisimpite FC kushoto wakati wa
michezo ya kusaka timu mbili za mkoa wa Dodoma zitazoshindana na
nyingine mbili za Morogoro ili kucheza ligi ndogo na kupata timu moja
itayowakilisha mashindano ya Castle Lager Perfect Six kutoka kanda ya
katika michezo iliyofanyika kwenye uwanja wa centel msikiti wa Gadaff
mjini Dodoma juzi ambapo katika mchezo Market FC ilishinda bao 2-1.
Ramadhan
Chinja wa timu ya Manzese kulis akipiga krosi dhidi ya Ally Maulid
kulia wa Santos wakati wa michezo ya kusaka timu mbili za mkoa wa Dodoma
zitazoshindana na nyingine mbili za Morogoro ili kucheza ligi ndogo na
kupata timu moja itayowakilisha mashindano ya Castle Lager Perfect Six
kutoka kanda ya Kati. Mchezo huo ulifanyika kwenye uwanja wa Centel
mjini Dodoma juzi ambapo katika mchezo Manzese iliibuka na ushindi wa
bao 3-1.
Ramadhan
Chinja wa timu ya Manzese (katikati) akipiga mpira huku mbele ya
wachezaji wa Santos Rashid Seif kushoto na Athaman Lukinda kulia wakati
wa michezo ya kusaka timu mbili za mkoa wa Dodoma zitazoshindana na
nyingine mbili za Morogoro ili kucheza ligi ndogo na kupata timu moja
itayowakilisha mashindano ya Castle Lager Perfect Six kutoka kanda ya
kati. Michezo hiyo ilifanyika kwenye uwanja wa Centel mjini Dodoma juzi
ambapo katika mchezo Manzese iliibuka na ushindi wa bao 3-1.
No comments:
Post a Comment