Mwandishi wa habari za michezo Ezra Kaaya (kushoto) akiubusu mpira wa Brazuca ambao utatumika kama mpira rasmi wa Kombe la dunia baada ya kukabidhiwa mpira huo kama zawadi na Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania, Fimbo Buttallah kwenye hafla ya kutangaza Castle Lager kama mdhamini rasmi wa matangazo ya luninga ya Kombe la Dunia kupitia SuperSport hapa nchini na Afrika nzima. Katikati ni Meneja wa Castle Lager, Kabula Nshimo.
Katika kuendeleza ushirikiano wake na chapa zinazoongoza duniani pamoja na matukio makubwa ya
michezo kimataifa, mwaka huu Castle Lager itakuwa itakuwa mdhamini wa matangazo ya luninga ya
Kombe la Soka la Dunia kupitia SuperSport, idhaa ya michezo inayoongoza barani Arika.
Udhamini huu unamaanisha kwamba Castle Lager itahakikisha wapenzi wa sokana wanywaji wa
Castle Lager barani Afrika wanafurahia matangazo bora ya shindano kubwa zaidi la soka duniani
ambalo litaanza mwezi huu nchini Brazil.
“Ikiwa ni chapa ambayo inafahamika kwa kujihusisha na mpira wa miguu barani Afrika, tumeona ni
vizuri kushirikana na SuperSport, idhaa ya michezo inayoongoza barani ili kuwaletea wanywaji wa
Castle Lager na wapenzi wa soka matangazo ya Kombe la Dunia moja kwa moja kutoka Brazil,”
alisema Fimbo Buttallah, Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania.
Vilevile, wanyawji wa Castle Lager na mashabiki wa soka wanatufaika kupitia promosheni mbalimbali
ambazo zitawapatia fursa ya kushinda safari kwenda Camp Nou huko Barcelona nchini Hispania
nyumbani kwa timu ya FC Barcelona na kukutana na baadhi ya wachezaji wa FC Barcelona ambao
watacheza kwenye Kombe la Dunia.
“Mara zote Castle Lager hujitahidi kuwapa wanywaji wake burudani zenye ubora wa kimataifa na
hii ni njia mojawapo ya kuwashukuru wanywaji wa Castle Lager kwa kutuunga mkono na wakati huo
huo tukitumia manufaa ya ushirikiano wetu na FC Barcelona kwa kuwapa nafasi ya kipekee kabisa
wanywaji wa Castle Lager kuwaona wachezaji kutoka sehemu mbalimbali duniani ambao wanaichezea
FC Barcelona, mojawapo ya klabu kubwa zaidi duniani,” amesema.
“Wakati Kombe la Soka la Dunia likikaribia, wanywaji wa Castle Lager wajitayarishe kwa promosheni
kabambe mbalimbali kutoka kwa bia yao waipendayo kwa ajili yao kushiriki na kujipatia nafasi ya
kukutana na baadhi ya wachezaji soka wawapendao,” alisema Kabula Nshimo, Meneja wa Bia ya
Castle Lager.
Ni dhahiri kwamba Castle Lager ni mdau mkubwa wa soka barani Afrika kwa miaka mingi, bia hii
imejikita katika kudhamini mchezo huu maarufu zaidi duniani katika ngazi mbalimbali,” Nshimo alisema.
Castle Lager imekuwa ikifahamika sio tu kwa kuwa bia inayoongoza barani Afrika lakini pia ikiwa ni
chapa ambayo huanzisha ubia na chapa nyingine zinazoongoza kwa ubora au matukio makubwa zaidi
duniani. Mwaka jana Castle Lager ilisaini mkataba wa ushirikiano kuwa bia rasmi ya FC Barcelona
barani.
No comments:
Post a Comment