HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 3, 2013

WIZARA YA UCHUKUZI YAADHIMISHA WIKI YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUSAFISHA KATIKA ENEO LA STESHENI YA TAZARA

Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira na Usalama, Bi. Tumpe Mwaijande akiongea na wafanyakazi wa Wizara na taasisi zilizo chini ya Wizara (hawapo pichani) hiyo baada ya kumaliza zoezi la usafi katika eneo la Buguruni Bahresa leo asubuhi. Pamoja na zoezi la Usafi Wizara ya Uchukuzi ilikabidhi Majembe, mafyekeo na reki kwa Shule ya Msingi Hekima na Zahanati ya Buguruni.
Wafanyakazi wa Wizara ya Uchukuzi na Taasisi zilizo chini ya Wizara wakiwa ndani ya Treni kuelekea katika kituo cha Buguruni Bahresa, ambapo waliadhimisha Wiki ya Mazingira Duniani kwa kufanya usafi katika eneo hilo leo asubuhi. Kauli Mbiu ya Wizara katika siku hii ni "Hifadhi maazingira kwa Uchukuzi Endelevu". Aidha Kauli mbiu ya Kitaifa ni 'Fikiri, kula; hifadhi Mazingira".
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), Mhandisi Aman Kisamfu (wa pili kutoka kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi (wa tano kutoka kushoto) wakisubiria kuanza kazi ya Usafi katika eneo la Stehseni ya Buguruni Bahresa. Wizara ya Uchukuzi na Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo wamefanya usafi kwenye eneo hilo leo asubuhi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani mbayo kitaifa inaadhimishwa Mkoani Rukwa.
Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira na Usalama wa Usafiri Majini, Bi. Tumpe Mwaijande (aliyeshika mfuko) akifanya usafi katika eneo la Buguruni Bahresa kama ishara ya kuadhimisha Wiki ya Mazingira Duniani. Wafanyakazi wa wizara ya Uchukuzi pamoja na taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo walifanya usafi katika eneo hilo kama ishara ya kuadhimisha siku ya Mazingira Duniani ambapo Kauli mbiu ya Wizara hiyo ikiwa ni "Hifadhi Maazingira kwa Uchukuzi Endelevu".
Wafanyakazi wa Wizara ya Uchukuzi na taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo wakifanya usafi katika Stesheni ya Buguruni Bahresa kama ishara ya kuadhimisha wiki ya Mazingira Duniani, Zoezi hilo la kufanya usafi limebeba kauli mbiu inayosema "Hifadhi Maazingira kwa Uchukuzi Endelevu".

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad