HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 20, 2013

Tambiko la kigogo lafanyika mkoani Dodoma

Chifu wa kabila la Kigogo,Lazaro Chihoma akimuonyesha Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini,Dkt. David Malole Historia ya kabila la kigogo iliyoandikwa kwenye Mnara uliojengwa pembezoni mwa kisima Cha Maajabu Kilichopo katika mlima Wa Bwibwi kijiji cha Iyumbu, wakati wa tambiko la wazee wa kabila hilo.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini,Dkt. David Malole akishuka ngazi kuingia kwenye Kisima cha Maajabu Kilichopo katika mlima wa Bwibwi uliyopo katika kijiji cha iyumbu Mbunge huyo ni Miongoni mwa watu 100 walioingia kwa pamoja kukishuhudia kisima hicho wakati wa tambiko la wazee wa kabila hilo.
Chifu wa Kabila la Kigogo,Lazaro Chihoma akiwa juu ya Mnara uliopo pembezoni mwa Kisima cha maajabu kilichopo katika mlima wa Bwibwi kijiji cha iyumbu manispaa ya Dodoma, uliondikwa hitoria ya kabila hilo wakati wa tambiko la mwaka huu ambalo hufanyika kila katikati ya mwaka.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini DKT. David Mchiwa Malole akimiminiwa Pombe ya Kienyeji na Mke wa Chifu wa kabila la kigogo,Luce Masuma Chihoma, kwaajili ya tambiko la kabila la kigogo lililofanyika katika kisima cha maajabu kilichopo katika mlima wa Bwibwi kijiji cha Iyumbu kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma. [PICHA NA JOHN BANDA]

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad