Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Kampuni ya bia ya Serengeti Mzee Mark Bomani akiwatambulisha watoto yatima Irene Joachim Katikati na Geofrey Yohana watakaopanda mlima Kilimanjaro katika kuhamasisha taasisi na mashirika mbalimbali kuchangia fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi nchini Tanzania hafla hii ilifadhiliwa na Geita Gold Mine.
Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi TACAIDS Fatma Mrisho (wa pili kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Kampuni ya bia ya Serengeti Mzee Mark Bomani na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Geita Gold Mine Omar Issa wakimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 15,000,000 Sister Adalbera Mukure wa Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea watoto yatima cha Moyo wa Huruma cha Geita wakati wa hafla maalum ya kukabidhi fedha hizo kwa mashirika mablimbali yanayopambana na ugonjwa wa ukimwi iliyofanyika Ijumaa kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es salaam fedha hizo zinakusanywa Mgodi wa Dhahabu ya Geita Gold Mine na washirika wake kwa kupanda mlima Kilimanjaro
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Geita Gold Mine Omar Issa, Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Kampuni ya bia ya Serengeti Mzee Mark Bomani na Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi TACAIDS Fatma Mrisho, wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa TACAIDS kutoka kulia ni Jumanne Issango Mkurugenzi wa Uraghibishi, Beng’i Issa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala na Moriss Lekule Mkurugenzi wa Mwitikio wa Taifa hafla hii ilifadhiliwa na Geita Gold Mine.
Mgodi
wa Geita umejiandaa na mwaka mwingine wa Kilimanjaro Challenge katika
Hotel ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam, Tanzania Ijumaa
iliyopita. Pia ufunguzi wa hafla huo ulihusisha kutaja majina ya asasi
zitakazo faidika na fedha zilizokusanywa katika upandaji mlima mnamo
mwaka wa 2012.
Mpango
huu kwa mara ya kwanza ulianzishwa mnamo mwaka 2002 ukihusisha
wapandaji mlima 47 uliowezesha kukusanya kiasi cha fedha za kitanzania
milioni 62. Ni mafanikio hayo yaliyoipa nguvu na moyo Geita Gold Mine
kufanya tukio hilo la upandaji mlima kama tukio la kitaifa la kila
mwaka. Tangu wakati huo wastani wa wapandaji 50 mpaka 55 walijiunga na
msafara huo kila mwaka. Hadi sasa, zaidi ya watu 500 kutoka duniani kote
wameshiriiki katika kukusanya zaidi ya fedha za Kitanzania Billioni 2
ambazo zimenufaisha zaidi ya asasi zisizo za kiserikali 30 NGO nchi
nzima katika kupambana na VVU/UKIMWI Tanzania.
“Lengo
la Kilimanjaro Challenge ni kujenga uelewa zaidi juu ya janga la
VVU/UKIMWI, kutoa msaada wa kifedha kwenye mpango huo na kujenga timu
bora ya kitaifa katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI.” Alisema Bwn.
Godvictor Lyimo.
Mpango
huu wa kujitolea na ule wa serikali unawapa nafasi wapandaji wa ndani
kupanda mlima Kimlimanjaro. Katika miaka 11 iliyopita watu wengi
wameshiriki katika kupanda mlima kwa kujitolea,akiwemo mvulana wa miaka
11 na mzee wa miaka 84, Raisi wetu Mstaafu Mhe. Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Kwa
mujibu wa Waziri mkuu Mhe. Mizengo K. Pinda, uamuzi uliofanywa na Mzee
Mwinyi ulikuwa ni wa kujidhatiti, akinukuu kauli ya ‘Mbiu ya Mgambo’
katika uamuzi huo. Kwa mujibu wa Bwn Godvictor Lyimo Mkurugenzi wa
Maswala ya Ndani GGM, “Imeripotiwa kwamba kiwango cha maambukizi
kimepungua kutoka asilimia 13 mwaka 2000 hadi asilimia 7.8 mwaka 2007 na
kwenda chini zaidi mpaka asilimia 5.1 mwaka huu 2013.
Kama
moja ya jitihada za kuongeza uelewa juu ya VVU/UKIMWI, Raisi Jakaya
Kikwete alizindua kampeni ya upimaji wa hiyari wa VVU/UKIMWI kwa kutumia
mwamvuli wa “Kilimanjaro Challenge” GGM mpango huu umepata mafanikio
katika kutoa uelewa juu ya janga hili na tunaangazia kuendeleza jitihada
hizi mpaka pale Tanzania itakapo tangaza kiwango cha maambukizi ya
UKIMWI ni sifuri.”
Migodi
ya Geita ipo kilometa nne Magharibi mwa Geita na Kasikazini Magharibi
mwa Tanzania. Mgodi unamilikwa na AngloGold Ashanti Limited kwa asilimia
100. AngloGold Ashanti Limited ni kampuni ya kimataifa inayojivunia
Afrika. Tunashughuli 20 ndani ya nchi kumi katika mabara manne , ikiwemo
ufunguzi wa miradi. AngloGold Ashanti ni moja ya makampuni makubwa ya
migodi ya madini ya dhahabu. Kwa habari zaidi tembelea:
www.anglogoldashanti.com
No comments:
Post a Comment