HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 23, 2013

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU TANGAZO LA AJIRA LILILOPO KATIKA MTANDAONI

Menejimenti ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) unapenda kuutaarifu umma wa Watanzania kuwa tangazo la nafasi za ajira ambalo limewekwa katika mtandao www.eastafricajobscarieer.com ni  batili. Mtandao huo ulichapisha tangazo hilo bila ridhaa ya Menejimenti ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya. Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya hauna mkataba wowote wa kibiashara na mtandao huo.

Aidha, tangazo hilo ni nakala ya tangazo la ajira ambalo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulilitangaza katika magazeti ya Mwananchi, Nipashe, na Daily News tarehe 07, 10 na 14 Februari, 2012 na mchakato wa kujaza nafasi zilizotangazwa ulishakamilika.

Menejimenti ya Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya inawaomba radhi wote ambao wamepata usumbufu kutokana na tangazo hilo.

Limetolewa na:
 Mkurugenzi Mkuu,
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,
S.L.P. 11360,
DAR ES SALAAM.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad