Mh. Alhaji. Adam Kimbisa
Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) wameapishwa rasmi kushika madaraka hayo huku Tanzania ikiwa na Wawakilishi tisa katika Bunge hilo.
Wabunge hao waliapa baada ya kupatikana Spika wa mpya wa Bunge hilo ambapo safari hii ikiwa ni Uganda kushika Uongozi huo wa Juu wa Bunge na Mwana Uchumi, Margareth Zziwa kuchukua nafasi hiyo.
Wabunge wote wa Tanzania katika Bunge la Jumuiya ya Mashariki waliokula kiapo hii leo ni pamoja na Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania kwenye Bunge EALA, Alhaj Adam Omar Kimbisa na Katibu wake, Mh Shy-Rose Saddrudin Bhanji.
Wengine ni Mhe. Anjela Charless Kizigha, Mh. Maryam Ussi Yahya,Mh.Nderkindo Perpetua Kessy, Dkt Twaha Issa Taslima, Mhe. Abdullah Ali Hassan Mwinyi, Mhe Bernard Musomi Murunyana Mhe. Charles Makongoro Nyerere na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta anaeingia kwa wadhifa wake wa Uwaziri.
Wabunge hao wameapishwa pamoja na wabunge wenzao wa Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Picha na FATHER KIDEVU BLOG
Mh. Samuel Sitta ni muwakilishi wa Tanzania
Mh. Abdullah Alli Hassan Mwinyi
Mh. Charles Makongoro Nyerere
Mh. Dkt. Twaha Issa Taslima
Mh. Nderkindo Perpetua Kessy
Mh. Bernard Musomi Murunyana
Mhe. Anjela Charless Kizigha

is a familly business gud on yu
ReplyDelete