HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, April 21, 2012

uvumi wa kujiuzuru kwa baadhi ya mawaziri haujathibitishwa hivyo mpaka sasa hauna ukweli wowote

Kwenye Mitandao kijamii ya Facebook, Twitter kwenye eGroups na eForums.kumekuwa na Taarifa za kujiuzuru kwa baadhi ya Mawaziri wa Wizara mbali mbali nchini lakini taarifa hizi zinatofautiana na kwa kuwa hazijathibitishwa kwa namna yoyote ile, zitabaki kuwa TETESI tu. Ikiwa ni kweli itafahamishwa hapo baadae kwani vipo vyanzo husika vinavyotakiwa kutoa taarifa hizo,hivyo taarifa hizi kwa sasa hazina ukweli wowote na zibakie kuwa ni tetesi tu na zipuuzwe!  

Unaweza kufuatilia mwenyewe kwenye ukurasa huu "bofya hapa"  utaona vijisanduku vya Twitter yenye tweets za Watanzania, JamiiForums, MabadilikoTanzania na Wanabidii.

Mojawapo inasema: "Wanaotajwa kujiuzulu ni Mkulo-Fedha, Dkt. Chami - Viwanda na Biashara, Dkt. Mponda - Afya na Nundu - Uchukuzi. Inasemekana watatoa tamko usiku wa leo."

    Joseph Msendo @msendo4life

    Breaking News ya Radio One, inasemekana mawaziri 8 wamejiuzulu..
    20 Apr 12

        * Reply
        * Retweet
        * Favorite

    Nathan Chiume @chiume

    Unconfirmed reports of forced resignations of 8 ministers in #Tanzania by MPs from ruling caucus after opposition no confidence vote threat
    20 Apr 12

        * Reply
        * Retweet
        * Favorite

    Edward Mhina @Mgossi

    RADIO ONE Breaking News: Inasema kwamba... Mhe.Jenista Mhagama ansema Wabunge wa CCM Wamefanya MAAMUZI MAGUMU usiku huu. Lakini HAJAFAFANUA!
    20 Apr 12

        * Reply
        * Retweet
        * Favorite

    Zitto Zuberi Kabwe @zittokabwe 20 Apr 12

    @Thuwein I claim no credit at all. Tunatimiza wajibu wetu. Players wengi, it was a teamwork @Semkae @Irenei2011 @iMashibe @AnnieTANZANIA

    Mbaraka Islam @Islam_Dar

    @zittokabwe @Semkae @MariaSTsehai @iMashibe Mkulo,Chami,Ngeleja, Nundu, Maige, Mkuchika, Maghembe Mponda barua usiku huu @ChangeTanzania
    20 Apr 12

        * Reply
        * Retweet
        * Favorite

Nyingine inasema: " Mawaziri hao ni; Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika, Waziri wa Kilimo Chakula na Ushurika Jumanne Maghembe na Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda."

Sababu ya kujiuzulu inatajwa kuwa ni kumnusuru Waziri Mkuu na taratibu nyingine zinazochukuliwa pale Waziri Mkuu anapojiuzulu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad