Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein akimfariji Mgonjwa Yassir Yussuf ambaye amepata ajali ya Pikipiki na kulazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar katika Uzinduzi wa Taifa wa Usalama Barabarani.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein akiwa katika matembezi pamoja na Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad kulia kwake,kushoto kwa Rais ni Rais wa Kitengo cha Usalama Barabarani wa Oman Balozi Wahid Alkharous walipokuwa wakielekea Hospitali ya Mnazi Mmoja ili kuwakagua wagonjwa waliokuwa wamepata ajali.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein
akitoa hotuba yake kuhusu Usalama Barabarani katika uzinduzi wa Taifa
wa Usalama Barabarani uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani
Mjini Zanzibar
Waziri
wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar,Hamad Masoud Hamad akitoa hotuba
kuhusu Usalama Barabarani katika uzinduzi wa Taifa wa Usalama
Barabarani kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Rais Shein kuhutubia katika
Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein
akivishwa Beji kuashiria Usalama Barabarani na Rais wa Kitengo cha
Usalama Barabarani wa Oman Balozi Wahid Alkharous katika Ukumbi wa
Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar leo katika hafla ya uzinduzi wa Taifa
wa Usalama Barabarani.






No comments:
Post a Comment