HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 1, 2011

KONGAMANO LA WANAHABARI LA BIMA YA AFYA MOROGORO LAMALIZIKA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni  (kushoto) akihutubia alipokuwa akifunga kongamano la wahariri na waandishi wa habari waandamizi kuhusu taarifa za tafiti za upatikanaji  wa huduma za afya zilitolewazo na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya   (NHIF) nchini. Kongamano hilo la siku mbili lilifanyika mjini Morogoro.
Mganga Mkuu wa Serikali, Mtasiwa akifafanua mambo mbali mbalimbali kuhusu masuala ya dawa na tiba.
 Mwenyekiti wa Kongamano hilo, Lauden Mwambona akiongoza  mijadala ya tafiti hizo. Kutoka kushoto ni Benny Mwaipaja wa TBC  Manyara na Saiboko wa Daily News.
Cosmas Nadimi wa MSD, akijibu maswali mbalimbali ya wanahabari  kuhusu usambazaji wa dawa nchini
Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emmanuel Humba akitoa majumuisho ya mapendekezo yaliyotolewa na wadau kwenye kongamano hilo.
 Blandina Nyoni akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Clement Mshana (kulia) pamoja na Mhariri  Mtendaji wa New Habari, Deodatus Balile. .
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni  (kushoto) akizungumza na wanahabari baada ya kufunga kongamano la  wahariri na waandishi wa habari waandamizi kuhusu taarifa za tafiti za  upatikanaji wa huduma za afya zilitolewazo na Mfuko wa Taifa wa Bima  ya Afya (NHIF) nchini. Kongamano hilo la siku mbili lilifanyika mjini  Morogoro.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika kongamano hilo mjini Moro.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad