HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 12, 2011

washiriki wa shindano la mama shujaa wa chakula wapewa somo la kilimo bora

 Mtaalam wa Kilimo toka Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) ,Dkt. Delphina Mamiro akitoa mafunzo ya kilimo kwa Kina Mama wanaoshiriki Shindano la Mama Shujaa wa Chakula linaloratibiwa na Shirika la Oxfam.Kina Mama hao ambao wameingia katika hatua ya kumi bora wapo kwenye kambi iliopo kwenye hoteli ya Rombo Green View,Sinza jijini Dar es Salaam.Mshindi katika Shindano hili atapata Trekta mpya atakalolitumia kwa kazi zake za kilimo.
 Mwakilishi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika ambaye pia ni jaji wa Shindano hilo,Bi. Joyce Mvuna akiwafafanulia jambo washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula,wakati semina ya Mafunzo ya Kilimo Bora inayoendelea kufanyika katika Hoteli ya Rombo Green View,Sinza jijini Dar es Salaam.Mshindi wa Shindano hili la Mama Shujaa wa Chakula atapata Trekta atakalolitumia katika kilimo.
 Mmoja wa washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula,Bi. Anna Olushuro akichangia mada wakati wa semina ya mafunzo ya kilimo bora yanayoendelea katika kambi yao iliyopo katika hoteli ya Rombo Green View, Sinza jijini Dar es Salaam.
Moja ya Kundi la Kina Mama walioingia katika hatua ya Kumi bora ya Shindano la Mama Shujaa wa Chakula,wakijadiliana jambo ambalo wataliwasilisha kwa makundi mengine na kuchangia mada kwa ujumla.kutoka kushoto ni Ruzena Binamu (Lind),Anna Olushuro (Morogoro),Getrude Anthony (Kagera) na Mwandiwe Makame (Kaskazini Unguja).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad