Wawakilishi toka Benki ya Dunia na Washiriki wa Maendeleo wakisiliza kwa makini mjadala wa Warsha ya Wadau wa Hifadhi ya Mazingira ya Ziwa Victoria (LVEMP 11) inayofanyika katika Hotel ya Imperial Botanical Beach Resort hapa Entebe Uganda. Wadau wa Maendeleo wamesisitiza umuhimu wa kuendelea na Hifandhi ya Maizingira na Utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Ziwa hilo.
Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia Maji shirikishi (Transboundary Waters) katika Wizara ya Maji Injinia Sylvester Matemu akitoa mada katika Warsha hiyo.Kulia Kwake ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Rasilimali za Maji katika Wizara ya Maji Injinia Naomi Lupimo.
Mtaalamu wa Benki ya Dunia anayeshughukilia Mawasiliano kanda ya Afrika Mashariki Bwana Steven Shalita akitoa maoni yake katika majadiliano na Wadau mabalimbali kwenye Warsha hiyo.Mwenye miwani kushoto ni Mratibu wa Mradi wa Hifadhi ya Mazingira ya Ziwa Victoria (LVEMP 11) kwa upande wa Tanzania Injinia Pius Mabuba.
Imperial Botanical Beach Hotel hapa Entebe amabako Warsha hiyo inafanyika.
Na Nurdin Ndimbe
Warsha ya Kimataifa ya Wadau wa Hifadhi ya Mazingira ya Ziwa Victoria inaendelea hapa Entebe Uganda kwa lengo la kutathimini maendeleo ya mradi huo ikihusisha Wadau, Makatibu Wakuu wa Wizara zinazohusika na Mradi huo toka Nchi za Afrika Masharki na pamoja na Wahisani wa Maendeleo wakiwemo Benki ya Dunia.
Washiriki wa Warsha wameomba watekelezaji wa Mradi sasa kuwa na nia ya dhati kabisa ya kuona kuwa maendeleo ya Miradi mabalimbali inakuwa endelevu kwa manufaa ya Wananchi wa Nchi hizo.
Hata hivyo Wadau wengi waliiomba Benki ya Dunia kupunguza urasimu katika masula yote yanayohusu Fedha na Manunuzi kwani, kwa maoni yao Miradi mingi inachelewa kuanza kwa sababu hiyo.
No comments:
Post a Comment