Mkurugenzi
Mtendaji wa Citibank Tanzania Jamal Hussein, akizungumza na Waandishi
wa Habari juu ya maandalizi ya mkutano wa Wafanyabiashara wa Afrika
Mashariki ambao utafanyika Hoteil ya Fairmont Mt. Kenya Safari Club,
Nanyuki nchini Kenya kuanzia tarehe 17 mpaka 20 Novemba mwaka huu. Mada
ya mkutano huo itakuwa ‘Ubunifu- chanzo cha ukuaji wa biashara Afrika
Mashariki’. Mkutano huo wa Waandishi wa Habari umefanyika leo Septemba
9, 2011 katika Hotel ya Movenpick jijini Dar es Salaam.
Bw.
Salim Bashir, ambaye ni kiongozi wa KPMG Tanzani, akizungumza na
Waandishi wa Habari juu ya maandalizi ya Mkutano wa Wafanyabiashara wa
Afrika Mashariki ambao utafanyika katika Hotel ya Fairmont Mt. Kenya
Safari Club, Nanyuki nchini Kenya kuanzania tarehe 17 mpaka 20 Novemba
mwaka huu. Mada ya Mkutano huo itakuwa ‘Ubunifu- chanzo cha ukuaji wa
biashara Afrika Mashariki. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Citibank Tanzania. Mkutano huo wa Waandishi wa Habari umefanyikaleo
Septemba 9, 2011 katika Hoteli ya Movenpick, Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu.
Maandalizi
ya mwaka huu ya mkutano wa wafanyabiashara wa Afrika Mashariki yameanza
ambapo zaidi ya viongozi wa makampuni makubwa 100 katika Ukanda huu
wanatarajiwa kushiriki.
Miongoni
mwa wanaotarajiwa kushiriki katika mkutano huo mkubwa ni pamoja na
viongozi wa makampuni kutoka Tanzania, Uganda, Rwanda na Kenya na
wanamatumaini kwamba biashara zao zitanufaika na ubunifu pamoja na fursa
zinazojitokeza katika Ukanda huu.
Akizungumza
na waandishi wa Habari katika Hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam,
Mwenyekiti mhamasishaji wa Tanzania, Bw.Jamal Hussein alisema mada ya
mwaka huu ni ‘Ubunifu- chanzo cha kuchochea ukuaji wa biashara Afrika
Mashariki’ ambapo taasisi na serikali zimeweka jitihada ya kufanya
Shirikisho la Africa Mashariki kuwa kivutio cha kukuza uchumi.
Bw.
Hussein alisema mkutano huo utafanyika Fairmont Mt. Kenya Safari Club
kuanzia tarehe 17 hadi 20 Novemba mwaka huu na huu ni mkutano wa tano
kufanyika, na utakuwa maalum kwa kujibu baadhi ya changamoto
zinazoathiri biashara katika Ukanda huu na kuzitafutia ufumbuzi .
‘Mkutano
wa mwaka huu unalenga kutumia mafanikio yake ya nyuma, na kutafuta njia
nyingine za kuendeleza na kukuza fursa zinazojitokeza katika ukanda huu
na Afrika kwa ujumla. Tunataraji kujua na kufahamu jinsi gani mikakati
na maamuzi ya viongozi yanaweza kuboresha ukuaji wa biashara’, alisema
Bw. Hussein.
Alisema
kuwa waandaji wa mkutano ujao (Citibank, Deloitte, KPMG, Nation Media
Group, PwC and Serena Hotels) hivi karibuni watataja wazungumzaji wa
ndani na wa kimataifa waliochanguliwa kwa kuzingatia uzoefu wao katika
ubunifu ili kuongoza mazungumzo wakati wa mkutano.
‘Tutawakutanisha
wafanyabiashara wenye uzoefu wa hali ya juu katika Ukanda huu. Lengo ni
kushirikisha umma na watu binafsi kwenye bara hili kwa ujumla ili
tuweze kuboresha uchumi wa Afrika Mashariki. Tutawataarifu
kinachoendelea kadri muda wa mkutano unavyokaribia’, alisema Bw.Salim
Bashir mshirika wa KPMG na mjumbe wa kamati ya maandalizi.
Mkutano
wa wafanyabiashara wa Afrika Mashariki ni jukwaa ambalo huwakutanisha
viongozi katika nyanja ya biashara Afrika Mashariki na kubadilishana
mawazo na maoni juu ya changamoto mbali mbali zinazowakabili na
kuangalia namna ya kuzikabili kwa pamoja.
Zaidi
ya viongozi 150 wa juu wa makampuni na taasisi muhimu za serikali
walihudhuria mkutano wa nne ambao ulifanyika mwaka 2008 Kampala, Uganda
chini ya mada: ‘Kukua kwa Ushindani Ndani ya Afrika Mashariki’.
Baadhi ya mambo muhimu yatakayozungumzwa wakati wa mkutano ujao ni pamoja na:
Kuzingatia
Ubunifu Katika Uchumi Unaokua, Vyombo vya Habari na Masoko, Kusimamia
Kipaji kwa Ubunifu, Kuwezesha Ubunifu (kifedha), changamoto za kisera;
Ushirikiano katika sekata za umma na binafsi;,Kushirikisjha Sekta
Binafsi Katika Uundwaji wa Sera za Umma, Kufanya Kipaji kupewa
kipaombele.
Katika
mikutano iliyopita, ikiwa ni pamoja na ule uliofanyika katika Hoteli ya
Ngurdoto nchini Tanzania mwaka 2004, na kuibua mipango mingi
inayotekelezeka kama vile Jumuiya ya Afrika Mashariki, kuimarisha
mawasiliano ya simu, kukuza kilimo; kushirikiana na mataifa mengine kwa
njia ya makubaliano ya miundombinu, na kuanzisha vituo vya utumiaji wa
wakala wa biashara. Mafanyikio makubwa kwa sasa ni kuwa na mkongo wa
bahari wa mawasiliano Afrika Mashariki.
No comments:
Post a Comment