HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, September 10, 2011

habari iliyotufukia hivi punde: watu zaidi ya 600 wahofiwa kufa maji kufuatia kuzama kwa meli ya mv spice island huko unguja

Taarifa iliyotufikia mapema leo kutoka huko visiwani Zanzibar,inataarifu kuwa Meli ya MV Spice Islands iliyokuwa safarini ikitokea Unguja kuelekea Pemba imezama katika mkondo wa Nungwi majira ya saa tisa za usiku wa kuamkia leo na kusadikiwa kusababisha vifo vya watu zaidi ya 600. 

Meli hii ambayo hubeba abiria na mizigo ambayo hufanya safari zake hizo kila siku, inasemekana ilikuwa na abiria 610 waliosajiliwa na hadi hivi sasa inadaiwa ni miili 100 tu iliyofanikiwa kuonekana na bado wataalam wa uokoaji wanaendelea kutafuwa miili mingine.

Mungu aziweke mahala pema peponi roho za ndugu zeru hao.

-Amein

 Tutaendelea kujulishana zaidi kadri taarifa zitakavyokuwa zikitufikia kutokea eneo la tukio.hivyo tendelee kuvuta subira.


===========================



Meli ya LCT SPICE ISLANDERS imebinuka na kuzama katika Bahari ya Hindi huko Pwani ya Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja ikielekea Pemba.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu, Mh Issa Haji Ussi akithibitisha tukio hilo amesema ajali  imetokea milango ya saa 8:30 za usiku wa kuamkia leo, na kuongezea kuwa  meli hiyo ilikuwa imebeba abiria 610 pamoja na mizigo.



Mh Ussi  amesema meli hiyo iliyokuwa imeondoka katika Bandari ya Malindi Unguja ikiwa katika hali ya uzima, lakini katikati ya safari ikapata hitilafu na kusababisha kubiruka na hatimaye kuzama.

Hadi sasa haijaweza kufahamika idadi kamili ya watu waliofariki,lakini vyombo vya uokozi vimefika katika eneo la tukio kutoa msaada.

Naibu Waziri  huyo  amesema Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya usafiri vya binafsi  vya boti ziendazo kasi zimekwenda eneo la tukio kutoa msaada unaohitajika, huku Jeshi la Polisi Tanzania limetuma Helikopta yake kwenye eneo la tukio.

Awali, amesema Mamlaka zinazohusika zilipata taarifa za kuzama kwa meli hiyo baada ya Meli ya Mv Jitihada inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuripoti kuzama kwa meli ya Spice Islanders ambayo ililazimika kukatisha safari yake kuelekea Kisiwani Pemba na kwenda kwenye tukio.

Serikali imesema taarifa zaidi zitakuwa zikitolewa na wananchi wameombwa kuwa watulivu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad