HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 22, 2011

Airtel Yafikisha huduma za mawasiliano katika vijiji 20 ndani ya mwezi mmoja mikoa ya Rukwa, Iringa, na Mbeya

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeendelea kuwafikishia wakazi  wa nyanda za kusini huduma za mawasiliano bora na kwa bei nafuu.

Airtel imefikisha huduma za mawasiliano katika vijiji vipatavyo 20 ndani ya mwezi mmoja vyenye idadi ya watu wapatao 52,775 ambao kwa kupitia mtandao wa Airtel wataweza kuboresha shughuli za  kilimo , biashara, katika kuinua uchumi wa jamii na nchi kwa ujumla.

Vvijiji vitakavyofaidika na huduma hizi ni Kaulolo, Nsenkwa,Mtakuja,Inyonga na Kamsisi mkoani Rukwa kwa Mkoa wa mbeya ni vijiji vya OldVwawa,Isangu,Ilolo,Ilembo,Mwantengo,Hasamba,Ukingani  Majengo, Mpangala,Kinyika,Ndapo,Nhungu,Matamba na Mahanji  wakati Mkoani Iringa ni Kibena, Tea estat.

Akiongea kwa niaba ya  kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Meneja Uhusiano wa kampuni ya simu ya Airtel Jackson Mmbando alisema” Mawasiliano ni muhimu katika kuboresha ulinzi, kukuza uchumi, kuweka jamii pamoja na kwa kutambua hilo, Airtel tumewekeza zaidi katika kupanua huduma zetu za mawasiliano hasa vijijini ambapo ndiko kwenye changamoto kubwa”.

Airtel tumeweza kuwafikishia huduma za mawasiliano kwa Wakazi wa maeneo ya Matamba  eneo maarufu kwa shughuli za kilimo na utalii, Pia tumewekeza kikamilifu na sasa mawasiliano bora yanapatika katika mbuga za KITULO zilizoko wilayani Rungwe mkoani Mbeya, wataliii sasa wataweza kuwasiliana na ndugu zao wakiwa katika ziara ya mbuga hizo aliongeza Mmbando.

Airtel inaendelea kupanua mtandao wake na kuwapatia wateja wake huduma bora na kwa bei nafuu zinazopatikana nchni nzima, lengo likiwa ni  katikati kutimiza dhamira yake katika kuwafikia wananchi wengi na kuboresha huduma za mawasiliano nchini hasa katika vijiji mbalimbali nchini

“Mkakati wetu wa kupanua mawasiliano vijijini unaendelea kwa kipindi chote cha Mwaka huu lengo letu ni kuhakikisha tunawafikishia wananchi wote huduma ya mawasiliano yenye utulivu zaidi na kutatoa uhuru wa mawasiliano zaidi  kwa wateja  kuendelea kufanya mawasiliano yenye manufaa yatakaowafanya wafurahie kutimiza miaka 50 ya uhuru wakiwa na miundombinu ya mwasiliano yanayojitosheleza” alimaliza kusemba Mmbando

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad