HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, June 16, 2011

SAUTI ZA BUSARA YAWAKUMBUSHA WASANII NCHINI KUCHUKUA FOMU ZA USHIRIKI MWAKANI



Mambo Mzee wa Mtaa kwa Mtaa.

natumai umzima na unaendelea na shughuli zako za kila siku kama kawaida,lengo la barua pepe hii kwanza ni kuunga mkono juhudi zako za kuuhabarisha umma kuhusu habari na matukio ya kila siku ya burudani.

Sauti za busara Zanzibar ni Taasisi isiyo ya kiserikali ambayo inajihusisha na uandaaji wa Tamasha la Muziki kutoka bara la Afrika na duniani kote ambalo linafanyika Zanzibar kila mwaka kati mwezi wa pili,mpaka sasa tunaelendelea kupokea maombi kutoka sehemu mbalimbali duniani katika matayarisho ya Tamasha letu la tisa ambalo litafanyika mwakani katika kisiwa cha Zanzibar.

Kutokana na maombi tuliyopata tumegundua kuna upungufu mkubwa sana wa maombi ya wasanii kutoka Tanzania kwa kuligundua hilo wiki iliyopita tuliamua kusambaza fomu zetu za maombi katka vituo vya redio,televishen,studio za kurekodi muziki vya Dares salaam ili iwe rahisi kwa wasanii kuwafikia.

Tukakaa tena tukaona si vibaya tukatumia baadhi ya blogs za burudani ili kuwakumbusha zaidi wasanii ambao wana nia ya kuchukua fomu au waliochukua kuwakumbusha kuzirudisha kwa sababu muda unakaribia kwisha.

Kwa maana hiyo tunakuomba utusaidie kuweka taarifa zetu kwenye Blog yako ili tupate wasanii wengi zaidi ambao watakapopata nafasi ya kushiriki itakuwa nafasi nzuri kwao kujitangaza kimataifa na kuutangaza muziki wa Tanzania.

Kwa kumalizia tunapenda kusema wote tuungane kuwasaidia wasanii wetu.

Ahsante
Journey A. Ramadhan
Project Coordinator
-- -- -- -- -- -- -- -- -- -- -- -- -- --
Busara Promotions,

PO Box 3635, Zanzibar,

Tanzania
+255 773 822 294 journey@busara.or.tz

www.busaramusic.org
Looking forwards... 9th

Sauti za Busara music festival,

8 - 12 February 2012

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad