HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, May 28, 2011

MISS UNIVERSE 2011 NI NELLY KAMWERA

Miss Universe 2011,Nelly Kamwera (kati) akiwa na mshindi wa pili,Neema Kilango (kulia) na Mshindi wa tatu,Yaceba Asenga mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Miss Universe 2011 yalifofanyika katika hoteli ya Golden Tulip,Masaki jijini Dar usiku huu.
Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania,George Rwehumbiza (kulia) na Meneja wa Mambo ya Nje wa Vodacom,Nector Foya wakiwa katika picha ya pamoja na Miss Universe usiku huu.
Mwanzilishi wa Mtandao wa Jamii Forums,Maxence Melo (kulia) na Mmoja wa wasaidizi wake,Bahati Chande wakiwa pamoja na top 3 ya Miss Universe usiku huu.
Miss Universe 2010 aliemaliza muda wake usiku wa leo,Hellen Dausen akimvisha Crown Miss Universe 2011,Nelly Kamwera ikiwa ni ishara na kukabidhima rasmi majukumu hayo ya ulimbwende.
Top 5 (anaekatika katikati yao ni MC Abby)
Mratibu wa shindano la Miss Universe,Maria Sarungi akitangaza washindi katika kinyang'anyiro hicho.
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation,Mwamvita Makamba akiuliza swali kwa mmoja wa washiriki wa Miss Universe wakati wa kipindi cha maswali na majibu.
Washiriki woote stejini.
Washindi wakiwa katika picha ya pamoja na Majaji.
Washindi wakiwa katika picha ya pamoja na wadhamini waliofanikisha shughuli nzima ya Miss Universe usiku huu.
Mie nikila konozz na Miss Universe 2011,Nelly Kamwera katika red carpet.
Wadau mbali mbali toka kila mahali walifika katika hoteli ya Golden Tulip usiku huu kushuhudia nani ananyakua taji la Miss Universe 2011.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad