HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, January 4, 2011

WAZIRI CHAMI KUTEMBELEA NCHINI INDIA KUHAMASISHA BIASHARA NA UWEKEZAJI

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Cyril Chami akihojiwa na waandishi wa ITV Ahmed Segule ( Mwenye Mic) na Godfrey Monyo( Wa kwanza kushoto). Waandishi hao na wa vyombo vingine, walipata fursa ya kuzungumza na Mh Waziri kuhusiana na malengo ya ziara yake ya siku 7 nchini India.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Cyril Chami akizungumza na waandishi wa Habari katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl JK Nyerere Jijini Dar es salaam jana, muda mfupi kabla ya safari yake kuelekea nchini India, ziara yenye lengo la kuhamasisha Sekta za Biashara na Uwekezaji nchini. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mh. Lazaro Nyalandu.


Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Cyril Chami, ameondoka nchini kuelekea nchini India kwa ziara ya siku saba ili kuhudhuria mkutano wenye lengo la kuhamasisha Biashara na Uwekezaji baina ya Tanzania na India.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kuondoka, Waziri Chami amesema, nia ya serikali ni kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya Tanzania na nchi rafiki pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini. Amesema akiwa nchini India, atazungumza na wafanyabiashara na taasisi mbali mbali za kibishara nchini humo ili ziweze kuja Tanzania kujionea fursa zilizopo na kuwekeza, hususan katika mamlaka ya EPZA.

Katika ziara hiyo iliyoandaliwa na taasisi ya Kamal Steel ya India yenye miradi mbali mbali nchini Tanzania, Waziri Chami ameongozana na Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya EPZA Dkt A. Meru. Ziara hiyo itamwezesha Mh Waziri kuhudhuria Mkutano wa kimataifa ujulikanao kama Global Commerece Chambers of Maharashtra utakaofanyika katika mji wa AURANGABAD katika jimbo la MAHARASHTRA.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad