Mkoa wa Mwanza umejipanga kuweka historia katika tasnia ya ulimbwende nchini kesho wakati wa kumpata mrembo atayewakilisha mkoa huo katika Miss Tz ya mwaka huu.
Kwanza kabisa imepania kuweka historia kwa kutetea taji la Miss Tanzania linaloshikiriwa na mrembo Nasreem Karim kutoka jijini Mwanza.
Pili ni kushirikisha mrembo mwenye ulemavu wa ngozi (albino) kwa mara ya kwanza katika historia ya mashindano hayo toka yaanze mwaka 1994, baada ya kupigwa marufuku baada ya kufanyika mara ya kwanza kabisa mwaka 1972 ambapo hayati Theresia Shayo aliibuka mshindi.
Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 23 si mwingine ila Grace Wabani ambaye ameleta msisimko wa waina yake katika kinyang'anyiro hicho, ikizingatiwa kwamba Mwanza ni mmoja wa mikoa inayoongoza kwa vitendo vya kikatili dhidi ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe.
Wachunguzi wa mambo wameielezea hatua ya mrembo Grace kushiriki katika mashindano ya ulimbwende ni mojawapo ya dalili za kufanikiwa kwa kampeni ya kuwajumuisha katika jamii albino ambao kutokana na imani potofu wamekuwa wakitengwa na kunyanyaswa pamoja na kufanyiwa unyama.
Wamesema Grace atazidisha mwamko kwa walemavu wenzie wa ngozi wajione kuwa na wao ni wanajumuiya na wanakubalika. Tayari hapa Dar kuna timu ya soka ya albino na pia kuna kikundi cha ngoma ambacho kilitumbuiza kwenye mashndano ya Miss Universe Tz wiki iliyopita.
Mratibu wa mashindano hayo kutoka kampuni ya Flora Entertaiment,Flora Lauwo amesema kuwa warembo wote wanaotarajia kushiriki kwenye mashindano hayo kesho ijumaa uwanja wa CCM Kirumba ni wakali na wametimia kila idara.
"Warembo wa safari hii ni wakali na wametimia kila idara,na kubwa zaidi kwa mara ya kwanza katika historia ya mshindano ya urembo hapa Tanzania na hata Afrika Mashariki kwa ujumla,safari hii tunamshiriki mwenye ulemavu wa ngozi (Albino) anayeitwa Grace Bani (23),ambaye naye kiukweli ana vigezo vyote vya kushiriki shindano hili,na nina imani naye atafanya vizuri",amesema Flora.
Flora amesema kuwa katika kinyang'anyiro hicho cha kumsaka kinara wa miss Mwanza 2009,washiriki wake wako jumla 15 akiwemo binti mwenye ulemavu wa ngozi (albino) Grace Wabani 23,
Aidha amewataja washiriki wengine kuwa ni Warembo wengine ni Miriam Ismail (18), Roda Uyombe (22),Jacquline Msuya (20),Miliam Gerald (21),Lisa Deus (20),Eva Sitta (22),Amina Adam (20),Aika Kanenda 21,Grace Frances 21 Fiobe Samweli (22), Sheila Ismail (19),Joy Pastory (20),Emi Yachi (22) na Bulelo Tambalo (20).
Katika shindano hilo Flora amesema kuwa pia kutakuwepo na burudani mbalimbali kama vile fasheni shoo,waimbaji wa muziki wa taarab akiwemo Hammer Q, Afua Suleiman, kikundi cha muziki wa kizazi kipya cha BWV cha jijini Mwanza na burudani nyinginezo.
Flora amesema ndani ya kinyang'anyir0 hicho kiingilio kimepangwa kuwa ni kiti cha Gold (20,000/=) kiti cha Silver (10,000/=) kiti cha kawaida 5000/=
Kwanza kabisa imepania kuweka historia kwa kutetea taji la Miss Tanzania linaloshikiriwa na mrembo Nasreem Karim kutoka jijini Mwanza.
Pili ni kushirikisha mrembo mwenye ulemavu wa ngozi (albino) kwa mara ya kwanza katika historia ya mashindano hayo toka yaanze mwaka 1994, baada ya kupigwa marufuku baada ya kufanyika mara ya kwanza kabisa mwaka 1972 ambapo hayati Theresia Shayo aliibuka mshindi.
Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 23 si mwingine ila Grace Wabani ambaye ameleta msisimko wa waina yake katika kinyang'anyiro hicho, ikizingatiwa kwamba Mwanza ni mmoja wa mikoa inayoongoza kwa vitendo vya kikatili dhidi ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe.
Wachunguzi wa mambo wameielezea hatua ya mrembo Grace kushiriki katika mashindano ya ulimbwende ni mojawapo ya dalili za kufanikiwa kwa kampeni ya kuwajumuisha katika jamii albino ambao kutokana na imani potofu wamekuwa wakitengwa na kunyanyaswa pamoja na kufanyiwa unyama.
Wamesema Grace atazidisha mwamko kwa walemavu wenzie wa ngozi wajione kuwa na wao ni wanajumuiya na wanakubalika. Tayari hapa Dar kuna timu ya soka ya albino na pia kuna kikundi cha ngoma ambacho kilitumbuiza kwenye mashndano ya Miss Universe Tz wiki iliyopita.
Mratibu wa mashindano hayo kutoka kampuni ya Flora Entertaiment,Flora Lauwo amesema kuwa warembo wote wanaotarajia kushiriki kwenye mashindano hayo kesho ijumaa uwanja wa CCM Kirumba ni wakali na wametimia kila idara.
"Warembo wa safari hii ni wakali na wametimia kila idara,na kubwa zaidi kwa mara ya kwanza katika historia ya mshindano ya urembo hapa Tanzania na hata Afrika Mashariki kwa ujumla,safari hii tunamshiriki mwenye ulemavu wa ngozi (Albino) anayeitwa Grace Bani (23),ambaye naye kiukweli ana vigezo vyote vya kushiriki shindano hili,na nina imani naye atafanya vizuri",amesema Flora.
Flora amesema kuwa katika kinyang'anyiro hicho cha kumsaka kinara wa miss Mwanza 2009,washiriki wake wako jumla 15 akiwemo binti mwenye ulemavu wa ngozi (albino) Grace Wabani 23,
Aidha amewataja washiriki wengine kuwa ni Warembo wengine ni Miriam Ismail (18), Roda Uyombe (22),Jacquline Msuya (20),Miliam Gerald (21),Lisa Deus (20),Eva Sitta (22),Amina Adam (20),Aika Kanenda 21,Grace Frances 21 Fiobe Samweli (22), Sheila Ismail (19),Joy Pastory (20),Emi Yachi (22) na Bulelo Tambalo (20).
Katika shindano hilo Flora amesema kuwa pia kutakuwepo na burudani mbalimbali kama vile fasheni shoo,waimbaji wa muziki wa taarab akiwemo Hammer Q, Afua Suleiman, kikundi cha muziki wa kizazi kipya cha BWV cha jijini Mwanza na burudani nyinginezo.
Flora amesema ndani ya kinyang'anyir0 hicho kiingilio kimepangwa kuwa ni kiti cha Gold (20,000/=) kiti cha Silver (10,000/=) kiti cha kawaida 5000/=
No comments:
Post a Comment