HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 27, 2009

Rais Kikwete Apangua Safu Ya Wakuu Wa Wilaya Nchini Na Kupanga Nyingine Mpya


Rais Jakaya Kikwete ameteua Wakuu wa Wilaya 15 ,  7 wamestaafishwa na  54  wamehamishwa vituo, ili kuongeza chachu ya  uwajibikaji katika kusimamia na kuratibu mipango mbalimbali ya maendeleo na uchumi ili kutimiza malengo ya serikali. 


Kwa mujibu wa taarifa toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Ma-DC wawili wamepangiwa kazi zingine na wawili wengine wamepangwa kufanya kazi katika jumuiya za chama tawala - CCM.



Walioteuliwa kwa mara ya kwanza ni  Ms Mercy Sila (Arumeru - Arusha), Mr Norman Sigalla (Hai – Kilimanjaro), Col Issa Njiku (Misenyi - Kagera), Ms Angelina Mabula (Karagwe - Kagera), Dr Rehema Nchimbi (Newala - Mtwara), Francis Isaac (Mbulu - Manyara), Lt Col Benedict K Kitenga (Rorya - Mara) na Lt Col Cosmas Kayombo (Mbarali - Mbeya). 


Wengine ni  Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba - Mwanza), Queen Mashinga Mulozi (Ukerewe - Mwanza), Fatuma Mwassa (Mvomero - Morogo), Fatma Ally (Nanyumbu - Mtwara), Juma Solomon Madaha (Tunduru - Ruvuma), Anatory Choya (Kishapu - Shinyanga) na  Erasto Sima (Korogwe - Tanga). 


Ma-DC waliostaafu ni  Elias Marugu (Misenyi - Kagera), Deusdedit Mtambalike (Muleba - Kagera), David Holela (Babati - Manyara), Hawa Ngulume (Mbarali - Mbeya), Mashiba H Mashiba (Kyela - Mbeya), Col Peter Madaha (Nyamagana - Mwanza) na  Gilbert Dololo (Kibaha - Pwani).  

Ma-DC waliopangiwa kazi zingine ni  Patrick Tsere aliyekuwa  DC (Ilala – Dar es Salaam), na  Doreen Kisamo (Uyui - Tabora). Mr Martin Shigela ambaye alikuwa DC (Lindi - Lindi) sasa ni Katibu Mkuu wa UVCCM ambapo  Husna Mwilima (Hai - Kilimanjaro) sasa ni Katibu Mkuu wa UWT.



Waliobadilishwa vituo ni pamoja na Elias W. Lali kutoka Arusha – Arumeru kwenda  Ngorongoro, Evans Balama toka Arusha – Arusha kwenda  Ilala, Jowiko W Kasunga  kutoka Arusha – Ngorongoro kwenda Monduli, Col Fabian I Massawe toka  Dar es Salaam – Kinondoni kwenda  Muleba, Abdallah A Kihato toka Dar es Salaam –Temeke kwenda  Kyela.

Wengine ni Zainab Kwikwega toka  Dodoma – Bahi kwenda Kasulu, Dr Ian J. Langiboli toka Dodoma – Chamwino kwenda Babati, Capt Seif A. Mpembenwe toka  Dodoma – Kondoa kwenda Handeni, Halima Dendego toka Dodoma – Mpwapwa kwenda Kilosa, Lephy B Gembe toka Iringa – Makete hadi  Chamwino na  Elaston J. Mbwilo toka  Iringa – Iringa kwenda  Mtwara.


Wengine ni Darry I Rwegasira toka  Iringa – Njombe kwenda  Mpwapwa, Said M Mkumbo toka Kagera – Chato kwenda Temeke, Frank A Uhahula toka  Kagera – Karagwe kwenda  Tarime, Lt Col John Mzurikwao toka Kigoma – Kibondo kwenda  Mpanda, Saidi Bwanamdogo toka  Kigoma – Kasulu kwenda  Kondoa, Raymond H Mushi toka Kilimanjaro – Rombo kwenda  Arusha.


Wengine ni Jordan Rugimbana toka  Kilimanjaro – Mwanga hadi  Kinondoni, Rashid M Ndaile toka  Lindi – Nachingwea kwenda Chunya, Anna Magowa toka  Lindi – Liwale kwenda  Hanang, Elias Goroi toka Manyara – Mbulu kwenda  Nachingwea, Capt Geoffrey Ngatuni toka  Manyara – Hanang kwenda Musoma.



Walohamishwa wengine ni Saveli Maketta toka  Mara – Musoma hadi Namtumbo, Stanley Kolimba toka  Mara – Tarime kwenda  Uyui, Ms Miriam L Lugaila toka  Mbeya – Rungwe hadi  Misungwi, Halima Kihemba toka  Mbeya – Mbozi kwenda  Kibaha, Fatuma L Kimario toka  Mbeya – Chunya kwenda  Igunga. 

Wengine ni  Athuman H Mdoe toka  Morogoro – Kilosa kwenda  Mwanga, Hawa Ng’humbi toka Morogoro – Mvomero hadi  Makete, Gishuli M Charles toka  Mtwara – Mtwara kwenda  Njombe, Jackson W Msome kutoka  Mtwara – Newala kwenda  Rungwe, Capt Assary Geofrey Msangi toka  Mtwara – Nanyumbu kwenda  Iringa.


Wengine ni Samwel Kamote toka Mwanza – Ilemela hadi Bukoba, Danhi Makanga toka  Mwanza – Kwimba kwenda Kibondo, Magalula S Magalula toka  Mwanza – Misungwi hadi  Lindi, Paul Chiwile toka Mwanza – Ukerewe kwenda Liwale, Mathew K Nasei toka  Mwanza – Magu kwenda Muheza, Lt Col Serenge M.  Mrengo kutoka Pwani – Bagamoyo hadi  Ilemela, Ali N Rufunga toka  Pwani – Rufiji kwenda  Manyoni.


Wengine ni Major Bahati Matala toka  Rukwa – Sumbawanga kwenda Kahama, Thobias Mazanzala toka Rukwa – Mpanda kwenda Sumbawanga, Gabriel Kimolo toka  Ruvuma – Namtumbo kwenda  Mbozi, Peter Toima Kiroya toka  Ruvuma – Tunduru kwenda  Rombo, Amina Masenza toka  Ruvuma – Mbinga kwenda Shinyanga.


Waliohamishwa vituo wengine ni Khadija R R Nyembo toka  Shinyanga – Kishapu kwenda  Chato, Col (rtd) Edmund Mjengwa toka  Shinyanga – Shinyanga kwenda  Mbinga, Magesa Mulongo toka Shinyanga – Bukombe kwenda Bagamoyo, Florence A Horombe toka  Singida – Singida kwenda  Bukombe, Pascal Mabiti toka  Singida – Manyoni kwenda  Singida, Cleophas Rugarabamu toka  Tabora – Igunga kwenda Nyamagana.


Wengine ni Kassim Majaliwa Majaliwa toka Tabora – Urambo kwenda  Rufiji, Lt Winfrid F Ligubi toka Tanga – Handeni kwenda  Urambo, Elizabeth Mkwasa toka Tanga – Korogwe kwenda  Bahi na Zainab Kondo toka  Tanga – Muheza kwenda Magu.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad