Wito huo umetolewa mapema leo akiwa mgeni rasmi Mkoani Morogoro wakati akizindua Baraza la Wafanyakazi wa TBS.
Mhe.Londo alisema baraza hilo linapaswa kuwa chombo chenye mchango chanya katika kuboresha mazingira ya kazi, kuimarisha ustawi wa wafanyakazi, na kuongeza ufanisi wa Shirika katika kutekeleza majukumu yake ya kisheria.
Alisema TBS ina jukumu nyeti la kuhakikisha bidhaa na huduma zinazozalishwa na kuuzwa nchini zinakidhi viwango vya ubora, usalama na ushindani katika masoko ya.ndani na ya kimataifa.
Alisema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kutambua na kuthamini nafasi ya Mabaraza ya Wafanyakazi kama vyombo muhimu vya kisheria vinavyolenga kuimarisha mahusiano mema kazini, kukuza majadiliano ya kijamii, na kuhakikisha haki na wajibu wa waajiri na wafanyakazi vinatekelezwa kwa uwiano na kwa maslahi mapana ya taasisi na Taifa.




No comments:
Post a Comment