HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, October 26, 2025

TMA YATOA TAHADHARI YA MVUA KATIKA MIKOA SABA

 


MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya uwepo wa mvua kubwa katika mikoa saba inayotarajiwa kunyesha kuanziq kesho.

Mvua hiyo inatarajiwa katika katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (pamoja na visiwa vya Mafia), Morogoro na Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya TMA, hali kama hiyo pia inatarajiwa kuendelea hadi keshokutwa (Jumanne) katika mikoa hiyo na kuongezeka hadi maeneo ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha.

Mamlaka imewataka wananchi kuchukua tahadhari na kufuatilia taarifa zitakazotolewa ili kuepuka athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad