Akifafanua lengo la kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi amesema kimejikita katika kujadiliana mikakati, kutoa ushauri na kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli za mazingira kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hizo na kuongeza tija katika sekta ya mazingira.
Viongozi hao pia wamejadili utekelezaji wa taratibu walizojiwekea katika kufuatilia na kusimamia Sheria za mazingira ili kuhakikisha rasilimali asilia zinatunzwa ipasavyo kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa ZEMA, Bw. Sheha Mjaja Juma amesisitiza umuhimu wa wananchi kutimiza wajibu wao kwa kufuata Sheria na taratibu za mazingira, sambamba na Taasisi za maendeleo kuhakikisha miradi yao inazingatia usimamizi endelevu wa mazingira ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi.
Itakumbukwa kuwa NEMC na ZEMA wamekuwa na mashirikiano ya muda mrefu na mara kadhaa wamekuwa wakitembeleana na kupeana uzoefu kwa maslahi mapana ya Mazingira nchini Tanzania.






No comments:
Post a Comment