HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, August 2, 2025

LUNA YANG’ARA KIMATAIFA KWA KUUNGA MKONO BIASHARA YA BIDHAA ZA KILIMO

 

 Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya LUNA Trading and Logistics Ltd imeendelea kupeperusha vyema bendera ya Tanzania baada ya kutunukiwa tuzo ya kuwa kampuni ya kwanza ya kizalendo nchini kwa mchango wake mkubwa katika kuunga mkono biashara ya bidhaa za kilimo duniani.

Tuzo hiyo imetolewa hivi karibuni na Afro World Agri-food International, taasisi inayotambua juhudi za taasisi na mashirika yanayochochea ustawi wa kilimo na biashara ya mazao ya kilimo katika bara la Afrika na kwingineko.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Mkurugenzi wa LUNA Trading and Logistics Ltd, Nuru Mmanyi, alisema tuzo hiyo ni uthibitisho wa dhamira ya kampuni hiyo katika kukuza uchumi wa kilimo kwa kusaidia wakulima kupata masoko ya uhakika kimataifa.

“Tumejikita kuhakikisha mazao ya kilimo kutoka Tanzania yanapata masoko ya nje ya nchi kwa bei shindani. Hili sio tu linawanufaisha wakulima bali pia linainua thamani ya mazao yetu katika soko la dunia,” alisema.

Aidha Mkurugenzi wa kampuni hiyo ameipongeza serikali kwa kuweka mazingira rafiki ya biashara hali inayopelekea kampuni za usafirisha nchini kustawi.
 

LUNA imekuwa ikisafirisha kwa mafanikio mazao mbalimbali ya kilimo kutoka Tanzania kwenda masoko ya nje, hasa katika nchi za Mashariki ya Kati, Ulaya, Asia na Amerika.

Bwana Mmanyi amsema ampuni hiyo inashirikiana kwa ukaribu na wakulima kupitia vikundi na vyama vya ushirika ili kuhakikisha mazao yanavunwa, kuchakatwa na kusafirishwa kwa viwango vya kimataifa.






 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad