Kikao hicho pamoja na mambo mengine kilijadili taratibu za Utatuzi wa Migogoro kati ya Wawekezaji na Serikali katika Mikataba ya Mataifa.
Kikao hicho pia kilijadili mageuzi yanayokusudiwa kufanywa katika Sheria za Kimataifa za biashara. Mageuzi yanayopendekezwa ni pamoja kuhakikisha Sheria za Biashara za Kimataifa zinajali maslahi ya mataifa yanayoendelea, Tozo na gharama zinazotolewa na Mabaraza ya Kimatifa zina uhalisia, Kuwepo kwa uwazi na ufanisi katika mwenendo wa Mashauri, na Kuwepo na uwezekano wa kukata rufaa kwenye maamuzi ya mabaraza ya Usuluhishi ya Kimataifa.
Kupitia kikao hicho Tanzania imesisitiza umuhimu wa kuweka taratibu za kushughulikia malalamiko ya wawekezaji mapema kabla haijawa migogoro (Mechanisms for prevention of Disputes).
Aidha, Tanzania kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeendelea kuwa mstari wa mbele kuchochea mageuzi kwenye utatuzi wa migogoro ya uwekezaji, kwa kusisitiza uwepo wa njia mbadala za utatuzi wa migogoro ikiwemo kutumia njia za upatanishi (amicable settlement).
Katika hatua nyingine, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametembelea Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania nchini Austria na kupokelewa na Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Austria Bw. Gerald Mbwafu, ambapo amemshukuru kwa mapokezi mazuri na kufanikisha ujumbe wa Tanzania kuhudhuria kikao hicho.




Kikao hicho pia kilijadili mageuzi yanayokusudiwa kufanywa katika Sheria za Kimataifa za biashara. Mageuzi yanayopendekezwa ni pamoja kuhakikisha Sheria za Biashara za Kimataifa zinajali maslahi ya mataifa yanayoendelea, Tozo na gharama zinazotolewa na Mabaraza ya Kimatifa zina uhalisia, Kuwepo kwa uwazi na ufanisi katika mwenendo wa Mashauri, na Kuwepo na uwezekano wa kukata rufaa kwenye maamuzi ya mabaraza ya Usuluhishi ya Kimataifa.
Kupitia kikao hicho Tanzania imesisitiza umuhimu wa kuweka taratibu za kushughulikia malalamiko ya wawekezaji mapema kabla haijawa migogoro (Mechanisms for prevention of Disputes).
Aidha, Tanzania kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeendelea kuwa mstari wa mbele kuchochea mageuzi kwenye utatuzi wa migogoro ya uwekezaji, kwa kusisitiza uwepo wa njia mbadala za utatuzi wa migogoro ikiwemo kutumia njia za upatanishi (amicable settlement).
Katika hatua nyingine, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametembelea Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania nchini Austria na kupokelewa na Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Austria Bw. Gerald Mbwafu, ambapo amemshukuru kwa mapokezi mazuri na kufanikisha ujumbe wa Tanzania kuhudhuria kikao hicho.




No comments:
Post a Comment