HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, June 22, 2025

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MAGEREZA NA VYUO VYA MAFUNZO WANOLEWA

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya waratibu, waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma. 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya waratibu, waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma. 

Meza kuu ikiwa katika mkutano huo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma. 


Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma.
Hakimu Denis John Mpelembwa akiwaapisha washiriki 

Washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma wakila kiapo cha kutunza siri kabla ya kuanza mafunzo hayo.
Mratibu wa Uandikishaji ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mafunzo , akizungumza jambo.
Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji, Caroline Ruben akiwasilisha mada kuhusu uraia kwa washiriki wa mafunzo hayo. 
******
Na. Waandishi Wetu
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewaasa watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye Magereza kwa Tanzania Bara na Vyuo vya Mafunzo kwa Tanzania Zanzibar kufanya kazi kwa weledi.
 
Wito huo umetolewa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa watendaji hao ambayo yameanza leo tarehe 22 Juni, 2025 Mkoani Dodoma kwa Magereza sambamba na Unguja kwa Vyuo vya Mafunzo. 

Akifungua mafunzo kwa watendaji hao yaliyofanyika Mkoani Dodoma kwa watendaji wa Magereza, Tanzania Bara, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Jacobs Mwambegele amesema Tume imewateua watendaji hao kutokana na weledi wao.
 
“Sina shaka kuwa kuteuliwa kwenu kunatokana na ujuzi, uwezo na weledi mlionao katika kutekeleza majukumu ya kitaifa likiwepo zoezi la uboreshaji wa Daftari ambalo ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025,” amesema Mhe. Mwambegele.
 
Amewahakikishia watendaji hao kuwa kwenye mafunzo hayo ya siku tatu Tume itawapa ujuzi wa kutosha kwa nadharia na vitendo kuwawezesha kutekeleza jukumu lao kwa weledi.
 
Akifungua mafunzo kama hayo Kisiwani Unguja, Zanzibar kwa watendaji wa Vyuo vya Mafunzo, Makamu Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufani Mstaafu, Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk ametoa wito kwa watendaji hao kuvitunza vifaa vya uboreshaji wa daftari.
 
“Ninatoa wito kwenu kuhakikisha mnavitunza vifaa vyote vitakavyotumika katika zoezi la uboreshaji wa Daftari na kuzingatia maelekezo yote yatakayotolewa na Tume ili muweze kuyafanyia kazi kwa usahihi wakati wote wa utekelezaji wa zoezi hilo,” amesema.
 
Jaji Mbarouk pia amewahakikishia watedaji hao kuwa maafisa kutoka Tume watakuwepo muda wote wa zoezi na kwamba endapo watapata changamoto ya aina yoyote wasisite kuwasiliana nao.
 
Kwa mujibu wa ratiba zoezi hilo la uboreshaji wa Dafatri kwenye Magereza na Vyuo vya Mafunzo linafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 28 Juni hadi tarehe 04 Julai, 2025 ambapo watakaohusika ni mahabusu na wafungwa walihukumiwa kifungo chini ya miezi sita.
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe, Jaji wa Rufani (Mstaafu), Mbarouk Salim Mbarouk 
akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya waratibu, waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa Vyuo vya Mafunzo kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 Mjini Unguja Zanibar. 
Mkurugenzi wa Ofisi ya Zanzibar, Ndg. Adam Mkina akizungumza wakati wa Mafunzo hayo.
Meza Kuu ikiwa katika mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad