Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) katika kikao chake cha 198 kilichofanyika chini ya Mwenyekiti wake CPA. Prof. Sylvia S. Temu imeidhinisha matokeo ya mitihani ya 101 ya Bodi kwa Watahiniwa waliofanya mitihani hiyo iliyofanyika mwezi Mei 2025 katika ngazi mbalimbali za masomo ya Bodi hiyo ya NBAA.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Elimu ya Taaluma na Mafunzo Peter Lyimo amesema kuwa matokeo hayo yameidhinishwa kufuatia mitihani iliyofanyika katika vituo 12 vilivyopo Tanzania Bara na Visiwani.
Amesema Jumla ya watahiniwa waliosajiliwa walikuwa 8,100 kati ya watahiniwa waliosajiliwa kufanya mitihani watahiniwa 845 sawa na asilimia 10.4 hawakuweza kufaya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali hivyo idadi ya watahiniwa waliofanya mitihani hiyo walikuwa 7,255 sawa na asilimia 89.6, kati ya hao watahiniwa 3,726 sawa na asilimia 51.4 walikuwa wanawake na watahiniwa 3,529 sawa na asilimia 48.6 walikuwa Wanaume.
Lyimo amesema jumla ya watahiniwa 466 wamefaulu mitihani ya Shahada ya Juu ya Uhasibu nchini yaani CPA (T). Kati ya watahiniwa hao wanawake ni 227 sawa na asilimia 48.7 na wanaume ni 239 sawa na asilimia 51.3 ambapo idadi hii inafanya jumla ya watahiniwa waliofaulu mitahani ya CPA kufikia 14,399 tangu mitihani hiyo ianze mwaka 1975.
Kati ya watahiniwa 466 waliofuzu kutunukiwa Cheti cha Taaluma ya juu ya Uhasibu wengi wao wametoka katika vyuo mbalimbali ambapo watahiniwa 95 sawa na asilimia 20.8 wametoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), watahiniwa 72 sawa na asilimia 15.8 wametoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), watahiniwa 66 sawa na asilimia 14.5 wametoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, watahiniwa 60 sawa na asilimia 13.2 wametoka Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA) na watahiniwa 19 sawa asilimia 4.2 wametoka Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.
Amesema jumla ya watahiniwa 11 wamefaulu mitihani ya CPA(T) linganifu (Equivalent Qualification) kati ya hao wanawake ni 04 sawa na asilimia 36.4 na wanaume ni 07 sawa na asilimia 63.6 ambapo mpaka sasa jumla ya watahiniwa waliofaulu mitihani hii wamefikia 341 tangu mitihani hii ianze Novemba 2014.
Pia amesema katika ngazi ya awali ya Uandishi na Utunzaji wa Hesabu(ATEC I) watahiniwa waliosajiliwa walikuwa 101 kati ya hao watahiniwa 07 sawa na asilimia 6.9 hawakuweza kufanya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali na hivyo watahiniwa waliofanya mitihani walikuwa 94 sawa na asilimia 93.1.
Pia ameeleza kuwa kati ya watahiniwa 94 waliofanya mitihani katika ngazi hii watahiniwa 78 ambao ni asilimia 83.0 wamefaulu mitihani yao na kati ya hao watahiniwa 30 sawa na asilimia 31.9 wanastahili kutunukiwa barua za ufaulu na watahiniwa 48 sawa na asilimia 51.1 wamefaulu baadhi ya masomo na watahiniwa 16 sawa na asilimia 17.0 hawakufaulu mitihani yao.
Aidha amesema katika hatua ya pili ya Cheti yaani ngazi ya uandishi na Utunzaji wa Hesabu(ATEC II) waliojisaliwa walikuwa 173 kati ya hao watahiniwa 19 sawa na asilimia 11.0 hawakuweza kufanya mitihani kutokana na sababu mbalimbali. Hivyo watahiniwa waliofanya mitihani walikuwa 154 sawa na asilimia 89.0.
“Kati ya watahiniwa 154 waliofanya mitihani katika ngazi hii watahiniwa 93 ambao ni asilimia 60.4 wamefaulu mitihani yao ambapo kati ya hao watahiniwa 31 sawa na asilimia 20.1 wanastahili kutunukiwa Barua za Ufaulu na watahiniwa 62 sawa na asilimia 40.3 wamefaulu baadhi ya masomo katika ngazi hii na watahiniwa 61 sawa na silimia 39.6 hawakufaulu mitihani yao” Alisema Lyimo
Amesema katika ngazi ya taaluma hatua ya awali watahiniwa waliosajiliwa walikuwa 1,077 kati ya hao watahiniwa 127 sawa na asilimia 11.8 hawakuweza kufanya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali hivyo watahiniwa waliofanya mitihani walikuwa 950 sawa na asilimia 88.2.
Pia ameeleza kuwa kati ya watahiniwa 950 waliofanya mitihani katika ngazi hii watahiniwa 730 ambao ni asilimia 76.8 wamefaulu mitihani yao ambapo kati yao watahiniwa 259 sawa na silimia 23.7 wanastahili kutunukiwa barua za ufaulu wa mitihani na watahiniwa 471 sawa na asilimia 49.6 wamefaulu baadhi ya masomo hivyo watahiniwa 220 sawa na asilimia 23.2 hawakufaulu mitihani yao.
Aidha amesema katika hatua ya kati waliojisaliwa walikuwa 4,094 kati ya hao watahiniwa 471 sawa na asilimia 11.5 hawakuweza kufanya mitihani kutokana na sababu mbalimbali. Hivyo watahiniwa waliofanya mitihani walikuwa 3,623 sawa na asilimia 88.5, kati ya watahiniwa hao 3,623 waliofanya mitihani katika ngazi hii watahiniwa 2,430 sawa na asilimia 67.1 wamefaulu mitihani yao kati ya hao watahiniwa 563 sawa na asilimia 14.8 wanastahili kutunukiwa barua za ufaulu na watahiniwa 1,894 sawa na asilimia 52.3 wamefaulu baadhi ya masomona watahiniwa 1,193 sawa na asilimia 32.9 hawakufaulu mitihani yao
Katika hatua ya mwisho, waliosajiliwa walikuwa 2,655 kati ya hao watahiniwa 221 sawa na asilimia 8.3 hawakuweza kufanya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali. Hivyo watahiniwa waliofanya mitihani walikuwa 2,434 sawa na asilimia 91.7. Kati ya watahiniwa 2,434 waliofanya mitihani katika ngazi hii watahiniwa 1,575 sawa na asilimia 64.7 wamefaulu mitihani mitihani yao ambapo kati ya watahiniwa 479 sawa na silimia 19.7 wanastahili kutunukiwa barua za ufaulu na watahiniwa 1,096 sawa na asilimia 45.0 wamefaulu baadhi ya masomo na watahiiwa 859 sawa na asilimia 35.3 hawakufaulu mitihani yao.
Lyimo amesema Bodi ya Wakurugenzi wa NBAA inatoa pongezi kwa wale wote waliofuzu mitihani yao na kuwataka wale ambao hawajafuzu kutokata tamaa badala yake waongeze bidii zaidi katika masomo yao ili wawezo kufuzu mitihani ijayo.
Pia amesema Bodi inawashauri watahiniwa kutumia vitabu vilivyotayayarishwa na Bodi katika kujiandaa kwa mitihani yao na pia wanashauriwa kusoma vitabu vingine vya ziada ili kuongeza ufahamu zaidi katika masomo hayo.
Mitihani ya muhula wa kati (Mid- session Examinations) itafanyika kuanzia Jumatatu tarehe 25 hadi Ijumaa tarehe 29 Agosti 2025 na mitihani ya Novemba itafanyika Jumanne tarehe 04 hadi Ijumaa tarehe 07 Novemba 2025 na pia matokeo ya mitihani ya 101 ya Bodi yanapatikana kwenye tovuti ya NBAA ambayo ni www.nbaa.go.tz.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Elimu ya Taaluma na Mafunzo wa NBAA Peter Lyimo
No comments:
Post a Comment