HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 2, 2025

DKT. YONAZI ATEMBELEA UWAKILISHI WA KUDUMU WA TANZANIA KATIKA OFISI ZA UMOJA WA MATAIFA GENEVA, AAZIMIA KUIMARISHA USHIRIKIANO

NA. MWANDISHI WETU – GENEVA USWISI

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi ametembelea Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Uswisi, ikiwa ni ziara yake ya kikazi nchini humo, lengo ni kushiriki Jukwaa la Nane la Dunia la Kupunguza Madhara ya Maafa linalofanyika kuanzia tarehe 2 hadi 6 Juni, 2025 Jijini Geneva Nchini Uswisi.

Dkt. Yonazi ameongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaoshiriki Mkutano huo huku akiambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Ofisi hiyo Bi. Stella Mwaiswaga, Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Charles Msangi pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Menejimenti ya Maafa sehemu ya Utafiti, Ofisi hiyo Bw. Vonyvaco Luvanda.

Aidha, amepokelewa na kufanya mazungumzo na Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa na Mashirika mengine ya Kimataifa Geneva Uswisi Mhe. Dkt. Abdallah Possi na kumweleza kuwa ushiriki wa Tanzania katika Jukwaa hilo unatija na manufaa makubwa kwa Taifa.

Alifafanua kuwa Jukwaa hilo linalenga kutathmini, kujadili maendeleo ya utekelezaji wake na kuimarisha masuala ya usimamizi wa maafa kimataifa kupitia makubaliano ya hiyari ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa ambayo yameridhiwa.

Sambamba na hilo, Dkt. Yonazi ameupongeza ubalozi huo na kuahidi kuendeleza ushirikiano masuala mbalimbali ili kuona fursa zilizopo Uswisi na kuzichangamkia fursa za kibiashara sambamba za zinazoendana na mabadiliko ya Kiteknolojia.

Akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa shughuli za ubalozi, Mhe. Dkt. Possi amesema amepongeza ushiriki wa Tanzania katika Jukwaa hilo la Nane na kusisitiza kuwa Tanzania ina kila sababu ya kuendelea kushiriki katika mikutano hiyo ili kuwa na mwendelezo mzuri utakaowezesha nchi kupata na kutumia fursa mbalimbali zinazotokana na Majukwaa hayo.






No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad