HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 1, 2025

WATUMISHI WA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TANZANIA KATIKA MAADHIMISHO YA MEI MOSI 2025

 

Watumishi Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC),makao makuu na Kampasi ya Dar es Salaam 
 wameshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ ambayo kimkoa yamefanyika katika wilaya ya Kinondoni kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es Salaam

Mgeni Rasmi wa maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Albert Chalamila ambapo amesisitiza kuwa wafanyakazi wanaposherehekea siku hii tutambue kwamba wao ndio wamebeba taswira ya serikali kwani mfanyakazi mmoja tu anaweza kusababisha serikali ichukiwe au ipendwe, hivyo wafanyakazi wote tuendelee kufanya kazi kwa uaminifu na imani kwani serikali inatujali na kutupenda.

Maadhimisho ya Mei Mosi 2025 yalikuwa na kauli mbiu isemayo ‘Uchaguzi Mkuu 2025 utuletee Viongozi wanaojali Haki na Maslahi ya Wafanyakazi, Sote Tushiriki’.

Baadhi Watumishi Chuo Cha Utumishi wa Umma wakipita mbele ya Jukwaa kuu huku wakiwa na bango lenye ujumbe kuhusiana Wafanyakazi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya  Watumishi Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dar es salaam  wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.















 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad